Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Saturday, February 29, 2020

Dkt. Ndugulile: Nchi iko salama dhidi ya Virusi vya Covid-19

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza jambo katika mahafali ya kidato cha sita katika Shule ya Mt. Maria Goreth mjini Moshi Februari 29, 2020. (Picha na Jabir Johnson) Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,...

Wasiozingatia usafi waendelea kutozwa faini Moshi

Wakazi wa Kata ya Bondeni katika Manispaa ya Moshi wametakiwa kuendelea kufanya usafi katika maeneo wanayoishi ili kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza yanayotokana na uchafu wa mazingira. Akizungumza na JAIZMELA NEWS Afrika Mtendaji wa kata hiyo Philipina Tenga alisema...

Mbowe akamatwa baadaya kumaliza mkutano, vurugu zaibuka Masama

Polisi Wilaya ya Hai wamemkamata Mbunge wa Hai kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe muda mfupi baada ya kumaliza mkutano wa hadhara katika viwanja vya Nkoromu Masama kati wilayani humo. Kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni...

Unaikumbuka siku Middlesbrough ilipowashangaza Bolton ya Jay Jay Okocha?

Februari 29, 2004 ilikuwa siku njema kwa klabu ya Middlesbrough ya England pale ilipovunja vitasa vya Bolton katika mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi.  Mabao mawili ya haraka yalitosha kuipa taji Middlesbrough. Na hilo lilikuwa taji lake la kwanza kubwa katika historia...

MAKTABA YA JAIZMELA: Elpidio Rivera Quirino ni nani?

Februari 29, 1956 alifariki dunia mwanasheria na mwanasiasa wa Ufilipino Elpidio Rivera Quirino Mwanasia huyo aliweka rekodi ya kuwa Rais wa Sita wa taifa hilo.  Alishika wadhifa huo kutoka mwaka 1948 hadi mwaka 1953.  Katika siasa za Ufilipino aliingia wakati...

Jenerali Delphin Kahimbi is no more

Naibu mkuu wa majeshi ya FARDC, Nchini DRC na Mkuu wa idara ya ujasusi katika jeshi Jenerali Delphin Kahimbi amepatikana amefariki dunia nyumbani kwake jijini Kinshasa jana asubuhi. Habari hiyo imetolewa na mkewe na washirika wenzake kadhaa wa karibu. Uchunguzi unaendelea,...

Friday, February 28, 2020

Nzige wavamia Mashariki ya DRC

Kwa sasa ni wilaya tu ya Aru katika mkoa wa Ituri, Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemocrasia ya Congo, iliyoathiriwa na nzige hao wa jangwani.  Lakini wadau mbalimbali katika nchi hiyo wanasema wana wasiwasi na uvamizi huo unaoendelea katika nchi mbalimbali...

Unaikumbuka siku chungu kwa mashabiki wa Paris Saint Germain?

Februari 28, 2010 makundi mawili hasimu katika soka nchini Ufaransa kundi la mashabiki wa klabu ya Paris Saint German walipambana tena na lile la Marseille ambapo yalisababisha kifo cha shabiki mmoja na wengine 20 kukamatwa katika vurugu hizo. Mchezo huo ulichezwa jijini...

MAKTABA YA JAIZMELA: Rajendra Prasad ni nani?

Februari 28, 1963 alifariki dunia Rais wa Kwanza wa kuchaguliwa wa India Rajendra Prasad. Mwanasiasa huyo ambaye alisomea sheria na sayansi ya siasa alishikia wadhifa huo kutoka mwaka 1950 hadi 1962. Prasad alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 78 huko Patna. Hali yake...

Thursday, February 27, 2020

Unaikumbuka siku iliyoweka historia kwa Maradona?

Februari 27, 1977 Argentina iliizabua Hungaria mabao 5-1 katika mchezo wa kirafiki ambao uliweka rekodi kwa mchezaji chipukizi wa Argentina Diego Maradona kuanza safari yake ya soka la Kimataifa akiwa na Albiceleste.  Maradona alikuwa na umri wa miaka 16 katika mchezo...

MAKTABA YA JAIZMELA: Boris Nemtsov ni nani?

Februari 27, 2015 alifariki dunia mwanasayansi na mwanasiasa wa Russia Boris Yefimovich Nemtsov. Nemtsov alikuwa mtaalamu wa Fizikia.  Katika siasa alikuwa kiungo muhimu katika kuanzisha ubepari katika ardhi ya Usovieti.  Alifanikiwa sana katika masuala ya...

Wednesday, February 26, 2020

Polisi Tanzania 1-1 Yanga SC: Walichinja Paka wakaambulia sare Ushirika

NA JABIR JOHNSON Februari 18, 2020 kulichezwa mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara katika dimba la Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.  Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya 1-1 baina ya wenyeji Polisi Tanzania na Yanga SC. Mabao ya Tariq Seif wa Yanga...

Unaikumbuka siku ya kwanza ya Roberto Carlos kuitumikia Brazil?

Februari 26, 1992 mlinzi wa kushoto wa Brazil Roberto Carlos aliiitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha timu ya taifa kwenye mchezo wa kirafiki ambao Seleccao walishinda kwa mabao 3-0 dhidi ya Marekani. Baada ya hapo alicheza jumla ya mechi 125 akiwa na Seleccao na...

MAKTABA YA JAIZMELA: Earl Lloyd ni nani?

Alhamisi ya Februari 26, 2015 alifariki mchezaji wa kikapu na wa kwanza Mmarekani Mweusi kucheza Ligi Kuu ya Kikapu nchini Marekani Earl Lloyd.  Nyota huyo alifariki akiwa na umri wa miaka 86.  Lloyd aliweka rekodi hiyo katika historia ya NBA mnamo mwaka...

Hosni Mubarak is no more

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak amefariki dunia jijini Cairo akiwa na umri wa miaka 91 katika hospitali ya kijeshi ya Al-Galaa. Hosni Mubarak alikuwa kiongozi wa Misri ambaye kwa karibu miaka 30 alikuwa nembo ya uthabiti katika eneo la Mashariki ya Kati kabla kulazimishwa...

Tuesday, February 25, 2020

Unaikumbuka Liverpool iliyotwaa Kombe la Ligi 2001?

February 25, 2001 katika Kombe la Ligi nchini England Liverpool na Birmingham City zilikutana katika fainali kwenye mchezo uliochezwa katika dimba la Millenium jijini Cardiff. Fainali hiyo ilikuwa ikiweka rekodi ya kuwa fainali ya 41 ya michuano hiyo  ambayo hushirikisha...

MAKTABA YA JAIZMELA: Jersey Joe Walcott ni nani?

Februari 25, 1994 alifariki dunia mwanamasumbwi  wa Marekani Jersey Joe Walcott.  Siku  aliyopoteza maisha ilikuwa Ijumaa, maradhi ya kisukari yalimuondoa nyota mwanamasumbwi huyo akiwa katika hospitali ya Our Lady of Lourdes Medical Center mjini Camden...