Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Friday, January 31, 2020

In memory of Rasual Butler and Leah LaBelle

Januari 31, 2018 alifariki dunia mchezaji wa kimataifa wa mchezo wa kikapu wa Ligi Kuu nchini Marekani (NBA) Rasual Butler.  Nyota huyo wa kikapu alikuwa mchezaji wa Miami Heat pia aliwahi kuhudumu na New Orleans Hornets, Los Angeles Clippers, Chicago Bulls, Toronto...

Thursday, January 30, 2020

MAKTABA YA JAIZMELA: Kwanini Mahtma Gandhi aliuawa?

Januari 30, 1948 alifariki dunia mwanasheria, mwanafalsafa, mwanaharakati wa haki za binadamu na kiongozi wa siasa nchini India maarufu Mahtma Gandhi.  Gandhi alipigwa risasi na kuuawa akitembea katika bustani ya nyumba huko Delhi. Mwuaji wake alikuwa Mhindu wa kundi...

Wednesday, January 29, 2020

Mateo Anthony aifumua Tanzania Prisons

Mshambuliaji wa Polisi Tanzania Mateo Anthony katika dimba la Ushirika, Moshi. Polisi Tanzania imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa katika dimba la Ushirika Mjini Moshi, Kilimanjaro. Bao la dakika...

MAKTABA YA JAIZMELA: Sheikh Ahmad Al-Jaber Al-Sabah ni nani?

Januari 29, 1950 alifariki dunia mtawala wa kumi wa taifa la Kuwait Sheikh Ahmad Al-Jaber Al-Sabah. Alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 65.  Sheikh Ahmad Al-Jaber Al-Sabah ni mtoto wa Jaber II Al-Sabah ambaye alikuwa mtawala wa Kuwait kati ya mwaka 1915 hadi...

Tuesday, January 28, 2020

Nike yaomboleza kifo cha Kobe Bryant

Kampuni ya vifaa vya michezo ya Nike imekuwa miongoni mwa makampuni yalioomboleza kifo cha nyota wa kikapu Kobe Bryant aliyefariki Januari 27, 2020 kwa ajali ya helikopta.  Ilichokifanya kampuni hiyo ni katika bidhaa zote zilizokuwa na zikitumiwa na Kobe Bryant na...

MAKTABA YA JAIZMELA: Meja Jenerali Suraj Abdurrhman ni nani?

Januari 28, 2015 alifariki dunia mwanajeshi na mhandisi wa majengo wa Jeshi la Nigeria aliyeongoza mapambano katika ardhi ya Liberia Meja-Jenerali Suraj Alao Abdurrahman.  Mwanajeshi huyo alifariki dunia jijini New York kwa ugonjwa ambao haukuwekwa wazi. Alisoma shule...

Monday, January 27, 2020

Kitambi Noma yatoa dozi yaizabua Moshi Veterans Club 3-2

Moshi Veterans Club wakiwa katika dimba la Ilboru Secondary School jijini Arusha kwenye warm up muda mchache kabla ya kuivaa Kitambi Noma katika mchezo wa kirafiki Januari 26, 2020. (Picha na Johnson Jabir)  Moshi Veterans Club imeshindwa kutamba katika mchezo wake...

Kobe Bryant na bintiye wafariki dunia katika ajali ya Helkopta

Nyota wa mpira wa kikapu nchini Marekani, Kobe Bryant amefariki dunia kwa ajali ya Helicopter iliyotokea jijini California, nchini humo. Bryant alikuwa akihudumu na Los Angeles Lakers inayoshiriki ligi kuu ya NBA nchini humo. Amefariki akiwa na umri wa miaka 41 na...

Kifo cha Suharto (1921-2008)

Januari 27, 2008 alifariki dunia mwanasiasa maarufu wa Indonesia ambaye aliwahi kushika wadhifa wa kuliongoza taifa hilo akiwa Rais wa pili. Huyu anafahamika kwa jina la Suharto. Alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 86.  Aliliongoza taifa hilo kutoka Machi 27,...

Saturday, January 25, 2020

Malameni Rock: Mwamba uliomaliza watoto wa Kipare

Malameni Rock at Mbaga, Same. Utamaduni ni jumla ya mambo yote yaliyobuniwa na jamii ili kukidhi utashi na maendeleo yake. Kwa maneno mengine utamaduni ni mwenendo wa maisha ya jamii, mtazamo wao wa mambo na taratibu zao za kuendesha maisha zinazowatofautisha wao na...

MAKTABA YA JAIZMELA: Mamadou Dia ni nani?

Januari 25, 2009 alifariki dunia Waziri Mkuu wa kwanza wa taifa la Senegal aliyefahamika kwa jina la Mamadou Dia.  Mwanasiasa huyo wa Senegal alihudumu katika nafasi hiyo kutoka mwaka 1957 hadi mwaka 1962. Alishika wadhifa huo hadi alipolazimishwa kujiuzulu na...

UN yataka usaidizi kukabiliana na nzige Afrika Mashariki

Umoja wa Mataifa umetoa wito wa usaidizi wa kimataifa kukabiliana na nzige wengi waliovamia maeneo ya Afrika mashariki. Msemaji wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa mataifa (FAO), ametoa wito wa kutolewa kwa msaada ili kukabiliana na athari za nzige kama vile...

Friday, January 24, 2020

Dkt. Mwakyembe: Serikali haitarudi nyuma wanahabari kuwa na Diploma

Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na wadau wa habari mkoani Kilimanjaro Januari 24, 2020 katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Mkoa. ...

Gazeti la Tanzania Daima Januari 24, 2020: Kangi Lugola

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli amemfuta kazi Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo Kangi Lugola, akisema wizara hiyo inaongoza katika kuchukua miradi ya ovyo. Rais Magufuli pia amemfuta kazi Kamishna wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini humo,...

Wanafunzi 24 waliotekwa Cameroon waokolewa

Jeshi la Cameroon limewaokoa wanafunzi 24 waliokuwa wakishikiliwa na waasi wenye silaha katika eneo linalozungumza Kiingereza la Meme nchini humo. Ofisa mwandamizi wa eneo hilo Ntou Ndong Chamberlain amesema, watoto hao walitekwa nyara mapema Jumanne kwenye shule yao...