Ad Code

Responsive Advertisement

Lesotho ni taifa la namna gani?

Ni taifa ambalo lipo katikati ya taifa jingine ikiwa na maana limezungukwa pande zote na taifa ya Afrika Kusini. 

Lesotho ni miongoni mwa mataifa matatu ambayo ni huru yakiwa yamezungukwa na taifa jingine na ni pekee nje ya Ulaya. 

Lesotho ina eneo linalochukua kilometa za mraba 30,000 likiwa na idadi ya takribani watu milioni mbili tu. Idadi hiyo ya watu ni makadirio ya mwaka 2016 yanayoipa kuwa nchi ya 144 ulimwenguni kwa kuwa na idadi kubwa ya watu. 

Mji mkuu ni Maseru. Hapo awali Lesotho ilikuwa koloni la Waingereza ikiitwa Basutoland. 

Ilipata uhuru wake kutoka kwa Waingereza Oktoba 4, 1966. Kutokana na kuwa na mamlaka kamili haikuwa  vigumu kutambuliwa na Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC). 

Kwa kifupi ni kwamba jina Lesotho lina maana ya ‘Ardhi ya Watu wanaozungumza Sesotho’. Wenyeji asilia wa taifa hilo ni Watu wa Jamii ya San ambao unaweza kuwafahamu kupitia sanaa zao zilizopo katika mawe kwenye ukanda wa milimani.  

Kuibuka kwa ufalme wa Moshoeshoe mwaka 1822 ambaye alikuwa mtoto wa Mokhachane aliyekuwa chifu mdogo kutoka ukoo wa Bakoteli kulitengeneza ukoo mkubwa ambao ulianza kuonekana mwaka 1804. 

Kati ya mwaka 1821 na 1823 wafuasi wa ukoo huo walianza kukaa katika milima ya Butha-Buthe wakiungana na wapinzani wao wa zamani dhidi Lifaqane kutoka milki ya Shaka Zulu kutoka mwaka 1818 hadi 1828. 

Mataifa mbalimbali Uingereza, Uholanzi na baadaye Ufaransa yalikuwa yakiliwania eneo hilo. Waingereza walikamata eneo hilo kutoka mwaka 1869 hadi kupata uhuru kwao mwaka 1966. Kwa sasa taifa hilo lina serikali yenye utawala wa kisheria wenye bunge lake. 

Waziri Mkuu wa Lesotho wa sasa ni Tom Thabane ambaye ni kiongozi mkuu wa serikali mwenye mamlaka ya juu nchini humo. 

Mfalme wa Lesotho ni Letsie III hana mamlaka ya juu Zaidi ya kuhusika katika masuala machache yasiyo ya kisiasa. Baraza la Seneti lina wajumbe 22 ambao ni machifu na wengine 11 wanaoteuliwa na Mfalme. 

Machifu huchukua nafasi hizo kwa urithi hivyo wanapokeza kwa taratibu za ukoo husika wa kichifu. Na wanaoteuliwa na mfalme hufanya kazi ya kumshauri Waziri Mkuu katika baadhi ya masuala nchini humo. 

Katiba ya Lesotho imechukua mfumo huru wa masuala ya kimahakama ikianzia chini mpaka juu Mahakama za Kijadi hadi mahakama ya Rufani. Lesotho imeundwa na wilaya 11 ambazo zinafanya uwepo wa tarafa 80 nchini humo na kata 129. 

Uchumi wa taifa hilo umejikita katika Kilimo, Ufugaji, Manufacturing na uchimbaji wa madini. Walio wengi hujikita katika kilimo. Madini ya almasi ndio yamekuwa yakichimbwa katika maeneo ya LetÅ¡eng, Mothae, Liqhobong, na Kao. 

Pesa inayotumika nchini humo ni Loti ambayo kwa thamani ya kitanzani Loti Moja ni sawa na shilingi 155 ya Tanzania. Asilimia 95 ya raia wa taifa hilo ni wakristo. 

Ripoti ya mwaka 2016 ilisema kuhusu muda wa kuishi wa binadamu katika taifa hilo inakadiriwa kuwa ni miaka 51 kwa wanaume na kwa wanawake ni miaka 55. Mwaka 2006 muda wa kuishi watu wa taifa la Lesotho ulikuwa ni miaka 42.

Post a Comment

0 Comments