Monday, February 20, 2017

Mtoto wa miaka saba aomba kazi Google

HEREFORD, ENGLAND
Chloe Bridgewater
Mtoto wa miaka saba ameomba kazi katika kampuni ya Google, kwa kumwandikia barua yenye maneno takribani 260 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hilo.
Mtoto huyo wa kike anayefahamika kwa jina la Chloe Bridgewater ambaye anaishi Hereford nchini England amemwandikia Mkurugenzi Mtendaji wa Google nchini Marekani Sundar Pichai kuwa anataka kufanya kazi.
Baba wa mtoto huyo Andy Bridgewater alimsaidia mwanaye kwa kuipeleka barua hiyo ambayo ilichapishwa kwenye gazeti la Bussiness Insider ikionyesha madhumuni ya mtoto huyo.
Mtoto huyo ambaye aliandika katika barua hiyo kuwa anapendelea kucheza na maroboti ambapo baba yake alimwambia kuwa ili aweze kujua zaidi atapaswa kujifunza kompyuta na mahali sahihi anapopenda ni Kampuni la Google.
Pia binti huyo alisisitiza kuwa ana uwezo mkubwa na walimu na baba yake wanamwambia kuwa ana akili darasani.
Barua ya Chloe Bridgewater kwenda Google
Kwa upande wao Google walimjibu binti huyo kuwa aendelee kuishi katika ndoto hiyo na wanatarajia kuwa atakapomaliza masomo wanasubiri barua ya kuomba kazi katika kampuni hilo.
Baba yake ni muuzaji wa majokofu na vifaa vyake


0 Comments:

Post a Comment