Wednesday, February 15, 2017

Mfumko wa bei wapanda Misri, watalii wapungua

CAIRO, MISRI     
Utalii nchini Misri umeshuka kutokana na thamani ya fedha kukosa thamani kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ajali ya ndege iliyotokea Oktoba 31, 2015 kwenye milima ya Sinai hivyo kukatisha safari za mashirika makubwa ya ndege.
Takwimu za Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), zimeonyesha bei za bidhaa nchini Misri zimepanda ghafla ukilinganisha na miaka iliyopita.
Kupanda kwa bei katika bidhaa mbalimbali nchini humo kumefika hadi asilimia 29.6 mwezi uliopita hivyo kuwa mfumko mkubwa kuwahi kutokea tangu Januari 2011.
Katika ripoti ya IMF imeonyesha Desemba mwaka uliopita nchini humo mfumko ulifika asilimia 24.3
Katika sekta ya utalii ambayo imekuwa muhimu kwenye upatikanaji wa fedha za kigeni imeshuka tofauti na ilivyotarajiwa.
Watalii nchini humo wamepungua nchini humo kutoka milioni 9.3 mwaka 2015 hadi milioni 5.3 mwaka jana.
Vyanzo vingine vinasema kupungua kwa watali nchini humo kumechangiwa na kuzuia kwa mashirika ya ndege ya Russia na Uingereza baada ya ajali ya ndege Oktoba 2015 kwenye milima ya Sinai.

Mkurugenzi wa IMF Chris Jarvis amesema walitarajia mfumko huo utajitokea na kwamba Misri imeanza vizuri kujipanga kuzuia kutokana na thamani ya pesa yake kushuka.

0 Comments:

Post a Comment