Tuesday, February 14, 2017

Vifo vya mapema India vyatisha

NEW DELHI, INDIA
Uchafuzi wa hali ya hewa kutoka viwandani.                    
UTAFITI wa kimataifa unaonyesha kuwa vifo vya mapema takribani milioni moja na laki moja nchini India vimetokea kutokana na uchafuzi wa hewa unaokua kwa kasi huku sikukuu za Diwali nchini humo zikichangia kwa kiasi kikubwa ongezeko hilo.
Aidha utafiti huo umebaini kuwa India itaipita China ambayo ilikuwa inaongoza kwa kutokea kwa vifo vya mapema kutokana na chembechembe hatari za PM2.5.
Taasisi ya Utafiti ya Boston  na ile ya Seattle nchini Marekani kwa pamoja zimesema karibu asilimia 50 ya vifo hivyo vimetokea kati ya mwaka 1990 na 2015.
Profesa Michael Brauer wa Chuo Kikuu cha British Columbia amesema kuwa kinachotokea India ni janga kubwa kutokana na uwekezaji mkubwa katika viwanda, kuongezeka kwa idadi ya watu na uwepo wa watu wenye umri mkubwa nchini humo.
Meneja wa Afya ya Mazingira na Jamii wa Taasisi ya utafiti wa sera za Afya nchini India Bhargav Krishna amesema uchafuzi wa hewa unaidhoofisha nchini hiyo kutokana na urasimu kuwa utungaji wa sera ambao serikali imekuwa iking’ang’ania kutoa mwongozo.
Marekani na Ulaya zimefanikiwa kwa kipindi hicho kupunguza asilimia 27 licha ya vifo vya mapema  kuwa 88,000 kwa Marekani na 258,000 barani Ulaya.
Asthma na vichomi vimekuwa changamoto kubwa hivyo kusababisha moyo kushindwa kufanya kazi yake vizuri kutokana na chembechembe zinazotoka kwenye magari na viwanda vinayotumia injini za dizeli pia vumbi la asili kuingia katika mishipa ya damu kupitia mapafu.
Idadi ya vifo vinavyotokana na uchafuzi wa hewa nchini India imeongezeka kutoka milioni 3.5 mwaka 1990 na kufikia milioni 4.2 mwaka 2015.
Msongamano wa magari katika jiji la New Delhi, India
CHANZO: CNN

0 Comments:

Post a Comment