Monday, February 20, 2017

Happy Birthday ya Robert Mugabe, kesho

HARARE, ZIMBABWE
Robert Mugabe
Kesho Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anatimiza miaka 93 ya kuzaliwa kwake huku akisisitiza kuwa hajamuona mtu sahihi wa kumkabidhi kijiti.
Kiongozi huyo aliyepo madarakani tangu walipojipatia uhuru mwaka 1980 amekaririwa akisema wanaopaswa kusema aondoke madarakani ni chama chake, lakini mpaka sasa Kamati Kuu imemtaka asimame kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.
Mugabe ambaye amekuwa mahiri kwa kauli kali ameongeza walio wengi katika nchi yake wanataka aendelee kwani hawaoni mbadala wa atakayepokea kijiti.
Hata hivyo amekana kuwa na matatizo ya kiafya licha ya kuwa na safari za mara kwa mara za kwenda Dubai na Singapore.
Katika hotuba amekuwa akisoma kwa muda mfupi na taratibu tofauti na walivyozoea. Ikumbukwe Septemba mwaka jana alisoma hotuba ambayo ilikuwa sawa na ile aliyoitoa mwezi mmoja kabla bila kujua, hali iliyoibua maswali kuhusu hali yake ya afya.
Aidha Mugabe alimsifia Rais wa Marekani Donald Trump kwa kuendelea kuimarisha sera za utaifa ambazo ameziita kuwa ni muhimu kwa maendeleo ya Zimbabwe.
Mugabe ambaye ni mwenyekiti wa ZANU-PF atasimama kwa uchaguzi wa mwaka 2018, ambapo juma lililopita mkewe Grace Mugabe aliibuka na kusema kuwa anaweza kuwa mtangulizi wake huku akikaririwa kwa kauli tata kuwa endapo Mungu ataamua Mugabe kufa basi wataipitisha maiti yake ipigiwe kura.
Endapo kiongozi huyo atachaguliwa na kumaliza muhula wake mwingine atafikisha miaka 100.

0 Comments:

Post a Comment