Tuesday, February 14, 2017

Makonda ataja moja akabidhi majina 97 ya wanaojihusisha na dawa za kulevya

NA PENDO MICHAEL
Gazeti la Habari Leo Februari 14, 2017 kuhusu Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kukabidhi majina 97
SIKU moja baada Rais John Magufuli kumwapisha Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga na kumtaka kusimamia kwa uadilifu mkubwa kwa mujibu wa sheria, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amemkabidhi majina 97 ya wanaojihusisha na biashara ya hiyo.
Hata hivyo Makonda alimtangaza mtu mmoja aitwaye Rashid Said maarufu Chidi Mapenzi akimtaka kufika Kituo cha Kikuu cha Polisi.
Makonda alimkabidhi majina hayo bila kuyataja katika hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere jana huku akisema malengo ya kuanzisha mapambano hayo ni kuwasaidia wahanga wa dawa hizo.
Katika siku za hivi karibuni Makonda amekuwa akilaumiwa na watu wa kada mbalimbali kwa namna anavyoendesha kampeni kupambana na dawa za kulevya, baada ya kitendo cha leo wadau mbalimbali wamesema huenda amepata ushauri na maoni ya namna ya kuendesha zoezi hilo.
Kwa upande wake Sianga ameahidi kutoa ushirikiano, na ameongeza kuwa atashughulikia kesi zote ambazo zimekuwa zikivurugwa na mahakimu.

Wengine waliokuwapo katika hafla hiyo ni Mchungaji George Fupe wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Sheikh Mkuu mkoa wa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Alhadi Mussa, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Simon Sirro.
Paul Makonda akizungumza jambo kuhusu dawa za kulevya.
Gazeti la Tanzania Daima Februari 14, 2017 kuhusu  Makonda na vita dhidi ya Dawa za Kulevya

0 Comments:

Post a Comment