Wednesday, February 22, 2017

NASA kutangaza 'Nje ya Mfumo wetu wa Jua'

NEW YORK, MAREKANI
Mchoro wa msanii ukionyesha sayari Kepler -452b
NA MWANDISHI WETU
Shirika la Anga za Juu la Marekani (NASA) leo linatarajiwa kutangaza ugunduzi "mkubwa" kuhusu mambo yaliyomo ‘Nje ya mfumo wetu wa jua’.

Hafla ya kutangaza ugunduzi huo itapeperushwa moja kwa moja kupitia runinga ya NASA na katika mtandao wa shirika hilo mwendo wa saa tatu Afrika Mashariki.

Habari kuhusu tangazo hilo pia zitachapishwa katika jarida la kisayansi la Nature na baadaye katika Reddit.

Mwaka 2015, Dkt Joe Michalski wa Makumbusho ya Historia ya mambo Asilia London alisema, "Duniani, popote unapopata maji, huwa kuna uhai."


Moja ya viashiria vya kuwepo na viumbe hai anga za juu au katika sayari nyingine ni uwepo wa maji.

CHANZO: BBC

0 Comments:

Post a Comment