Monday, February 27, 2017

Mauzo soko la Hisa yaongezeka

NA STELLA JOSEPH
Soko la Hisa
Mauzo katika soko la hisa yameongezeka kwa shilingi Bilioni 8.5 kutoka shilingi milioni 228 kwa juma lililopita ukilinganisha na shilingi Bilioni 8.6 kwa juma linaloishia Februari 24.
Meneja Mauzo wa Soko la Hisa na Biashara (DSE), Patric Msusa amesema idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imeongezeka kutoka hisa laki mbili elfu na hamsini na saba hadi hisa milioni 1.2
Amesema kutokana na ongezeko la bei za hisa, ukubwa wa mtaji wa soko umepanda kwa takribani shilingi Bilioni 100 kutoka shilingi Trilioni 20.
Amesema kiashiria cha kampuni zilizoorodheshwa katika soko yaani DSEI kimepanda kwa pointi 14 kutoka pointi 2294 hadi pointi 2308 kutokana na ongezeko la bei za hisa zilizoingia sokoni.
Sekta ya huduma za kibiashara (CS) imebaki kama awali huku sekta ya viwanda ikipanda kwa pointi 340 kutoka pointi 4194 hadi pointi 4534  na sekta ya huduma ya  kibenki na kifedha (BI) ikishuka kwa pointi 100 kutoka pointi 2642 hadi 2542.

0 Comments:

Post a Comment