Tuesday, February 21, 2017

Happy Birthday Robert Mugabe

Robert Mugabe
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anatimiza miaka 93 ya kuzaliwa kwake (Alizaliwa Februari 21, 1924). Mugabe amekuwa akijulikana kwa kauli kali tangu alipoipa uhuru nchi hiyo mwaka 1980.
Jina lake halisi ni Robert Gabriel Mugabe, Baba yake alikuwa fundi seremala na mama yake Bona alikuwa mtumishi wa kanisa akihudumia watoto. Katika familia yao walizaliwa  sita Miteri (Michael), Raphael, Robert, Dhonandhe (Donald), Sabina na Bridgette.
Alimwoa mwanadada Sally Hayfron mwaka 1967 aliyedumu naye hadi mwaka 1992 alipofariki.
Mwaka 1996 alimwoa Grace Marufu ambaye anaishi naye hadi sasa.
Aprili 17, 1980 alikabidhiwa kijiti cha kuwa Waziri Mkuu wa taifa hilo. Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye uwanja wa Rufaro allitangaza rasmi kuwa haitaitwa Rhodesia ya Kusini bali itaitwa Zimbabwe.
Kiongozi huyo ambaye kwa sasa anashikilia rekodi ya kukalia kiti hicho kwa muda mrefu tangu mwaka 1987  kwa tiketi ya ZANU-PF.
Mwaka 1980 hadi 1987 alikuwa Waziri Mkuu wa taifa hilo.
Mugabe ni wa kabila la Washona. Alizaliwa kutoka kwenye familia maskini ya Kutama nchini humo wakati huo ikiitwa Rhodesia ya Kusini.
Alisoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare na baadaye kuwa mwalimu katika nchi ya Zambia na Ghana.


0 Comments:

Post a Comment