Thursday, February 16, 2017

Gereji ya kurekebisha vifaa vya kijeshi yazinduliwa

PHNOM PENH, CAMBODIA

Gereji ya Vifaa vya Kijeshi iliyojengwa kwa msaada wa Serikali ya China imezinduliwa nchini Cambodia.Ujenzi wa gereji hiyo ambayo itatumika kurekebisha vifaa vya kijeshi ilianza kujengwa mwaka 2015.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Cambodia Jenerali Tea Banh akiwa na Balozi wa China nchini humo Xiong Bo wamezindua gereji hiyo katika Kikosi magari ya kijeshi Namba 99 kilichopo mjini mkuu Phnom Penh. Taarifa kutoka nchini humo zinasema gereji hiyo yenye teknolojia mpya ina ukubwa mita za mraba 500 ambayo itakuwa muhimu kwa Jeshi la Ulinzi la nchini hiyo. Uhusiano wa Cambodia na China uliimarika baada ya kumalizika kwa vita ya Cambodia na Vietnam mwaka 1991.

Wakati huo huo takwimu zinaonyesha kubwa idadi kuwa ya Wachina imekuwa ikiongezeka katika nchi ya Ukraine kutokana na urahisi wa kupata viza na uhusiano wake na taifa hilo la Ulaya. Takwimu hizo za Ukraine zimeonyesha raia wa China 20,555 wamezuru nchi hiyo mwaka jana ikilinganishwa na 13,602 mwaka 2015. Tangu Juni 2016 Ukraine ilianza kutoa viza ya siku 15 kwa wafanyabiashara na watalii raia wa China waliokuwa wakifika nchini humo kwa kutumia uwanja wa ndege wa Kiev Boryspil. Miezi minne baadaye Ukraine iliweza kutunga sera ya kuongeza matumizi ya viza hiyo hadi mji wa Odessa ulio kusini mwa Bahari Nyeusi.

0 Comments:

Post a Comment