Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Tuesday, February 28, 2017

Mabaraza la Madiwani Mkalama, Singida latimua watumishi

NA MWANDISHI WETU Mkalama, Singida; Mei 2016 (Picha na Maktaba) BARAZA la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida limewafukuza kazi watumishi wake watatu na kumsimamisha kwa muda mmoja kwa tuhuma mbalimbali, ikiwamo utoro kazini. Mwenyekiti wa...

Mwisho wa 'viroba' Machi 1

NA MWANDISHI WETU January Makamba SERIKALI imewataka wazalishaji  na wafanyabiashara kuacha kuilalamikia kwa hatua iliyochukua ya kutangaza marufuku ya uzalishaji, usambazaji na matumizi ya viroba kuwa imekuja ghafla huku wakijua kwamba tamko hilo lilitolewa tangu...

Google yakubali mchango wa ‘Malaika wa Rehema’ Abdul Sattar Edhi

CALIFORNIA, MAREKANI Abdul Sattar Edhi enzi za uhai wake KAMPUNI ya Google iliyo maarufu kwa utoaji wa huduma za intaneti na bidhaa zake imemkumbuka mwanzilishi wa Edhi Foundation aliyejitolea maisha yake kuwasaidia watoto maskini tangu akiwa na miaka 20 kwa kuchapisha...

Monday, February 27, 2017

Waziri Mkuu Majaliwa kufanya uzinduzi Feb 28

NA MWANDISHI WETU Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Kassim Majaliwa kesho atafungua mkutano wa siku moja wa Watendaji Wakuu na Wenyeviti wa Bodi za Mashirika ya Umma utakaojadili nafasi za Mashirika ya Umma katika utekelezaji...

Mauzo soko la Hisa yaongezeka

NA STELLA JOSEPH Soko la Hisa Mauzo katika soko la hisa yameongezeka kwa shilingi Bilioni 8.5 kutoka shilingi milioni 228 kwa juma lililopita ukilinganisha na shilingi Bilioni 8.6 kwa juma linaloishia Februari 24. Meneja Mauzo wa Soko la Hisa na Biashara (DSE), Patric...

'Nokia 3310' New Model yazinduliwa

BARCELONA, HISPANIA Toleo jipya la Nokia 3310  KAMPUNI ya simu za Nokia imeingia tena sokoni kwa kuishangaza dunia baada ya kutambulisha toleo za zamani la simu yao Nokia 3310 ambayo lilikuwa maarufu sana mwanzoni mwa karne ya 21. Aina hiyo ya simu kwa ukanda wa...

Saturday, February 25, 2017

Facebook yakiri kusaidia mkutano wa Republican

MARYLAND, MAREKANI Mark Zuckerberg wa Facebook WAKATI washauri wa juu wa Rais Donald Trump wakisisitiza kuwa wataendelea kumshawishi kiongozi huyo wa Marekani kutekeleza ahadi zake alizoahidi wakati wa kampeni, imeelezwa Facebook ilichanga dola 62,500 za Marekani kufanikisha...

Friday, February 24, 2017

'iPhone 8' njiani mwaka huu

CALIFORNIA, MAREKANI Kampuni linalojihusisha na kusanifu, kutengeneza, kuendeleza na kuuza kwa wateja vifaa vya elektroniki, programu za kompyuta na huduma za mtandao la Apple linatarajia kutoa simu iPhone 8 baadaye mwaka huu. Hayo yanajiri ikiwa leo ni siku ya kuzaliwa mwanzilishi...

Wafanyabiashara Sukari ya Magendo Mbeya wakamatwa, wapigwa faini

NA MWANDISHI WETU Sukari ya Kilombero katika pakiti zake Zaidi ya shilingi milioni tisa zimekusanywa na wakala wa vipimo mkoani Mbeya baada ya  kupigwa faini wafanyabiashara waliokamatwa wakiuza sukari iliyofungashwa katika ujazo usiokubalika kisheria. Kwa mujibu...

Thursday, February 23, 2017

King Salman kuzuru Indonesia

JAKARTA, INDONESIA Mfalme Salman wa Saudia Arabia Indonesia imetangaza kuwa Mfalme Salman wa Saudia Arabia atazuru nchi hiyo mapema mwezi ujao akiwa na ujumbe watu 1,500. Taarifa nyingine zinasema ufalme huo unatarajia kutumia mabilioni ya pesa kwa ajili ya kukaa kwenye...

Yoweri Museveni, Danny Faure kuzuru Tanzania

NA FELISTA HENRY Yoweri Museveni, Rais wa Uganda WAKAZI wa jiji la Dar es Salaam wametakiwa kutumia fursa ya kibiashara kupitia ujio wa viongozi wa juu wa Uganda na Visiwa vya Shelisheli kwa maendeleo ya nchi. Rais wa Uganda Yoweri Museveni na Danny Faure wa Ushelisheli...

Vifungashio vipya kutengenezwa Tanzania

NA MWANDISHI WETU Nembo ya Toyo Seikan Group Kampuni ya Toyo Seikan Group Holding Ltd kutoka nchini Japan imeonyesha dhamira ya kuwekeza nchini kwa kuzalisha vifungashio vya vinywaji vilivyotengenezwa kwa teknolojia ya kisasa na maofisa wa kampuni hiyo walio nchini kwa...

Wednesday, February 22, 2017

Raia 14 wa India wapandishwa kortini Kisutu

NA MWANDISHI WETU Raia wa India wafanyakazi kwenye Kampuni la Quality Group Ltd wakiwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Februari 22, 2017. Raia wa 14 wa India ambao wanafanya kazi Quality Group wamefikishwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi...

NASA kutangaza 'Nje ya Mfumo wetu wa Jua'

NEW YORK, MAREKANI Mchoro wa msanii ukionyesha sayari Kepler -452b NA MWANDISHI WETU Shirika la Anga za Juu la Marekani (NASA) leo linatarajiwa kutangaza ugunduzi "mkubwa" kuhusu mambo yaliyomo ‘Nje ya mfumo wetu wa jua’. Hafla ya kutangaza ugunduzi huo itapeperushwa...

Shahidi Namba 5 kesi ya Scorpion atinga mahakamani leo

NA MWANDISHI WETU Salum Njwete (katikati) akitoka katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Oktoba 19, 2016 USHAHIDI wa kesi inayomkabili Salum Njwete maarufu Scorpion umeendelea kusikilizwa leo katika mahakama ya wilaya ya Ilala huku shahidi wa tano ambaye ni daktari akidai...

Tuesday, February 21, 2017

Happy Birthday Robert Mugabe

Robert Mugabe Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anatimiza miaka 93 ya kuzaliwa kwake (Alizaliwa Februari 21, 1924). Mugabe amekuwa akijulikana kwa kauli kali tangu alipoipa uhuru nchi hiyo mwaka 1980. Jina lake halisi ni Robert Gabriel Mugabe, Baba yake alikuwa fundi seremala...

Monday, February 20, 2017

Happy Birthday ya Robert Mugabe, kesho

HARARE, ZIMBABWE Robert Mugabe Kesho Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anatimiza miaka 93 ya kuzaliwa kwake huku akisisitiza kuwa hajamuona mtu sahihi wa kumkabidhi kijiti. Kiongozi huyo aliyepo madarakani tangu walipojipatia uhuru mwaka 1980 amekaririwa akisema wanaopaswa...

Mtoto wa miaka saba aomba kazi Google

HEREFORD, ENGLAND Chloe Bridgewater Mtoto wa miaka saba ameomba kazi katika kampuni ya Google, kwa kumwandikia barua yenye maneno takribani 260 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hilo. Mtoto huyo wa kike anayefahamika kwa jina la Chloe Bridgewater ambaye anaishi Hereford nchini...

Friday, February 17, 2017

Makonda ni nani?

...

Thursday, February 16, 2017

Gereji ya kurekebisha vifaa vya kijeshi yazinduliwa

PHNOM PENH, CAMBODIA Gereji ya Vifaa vya Kijeshi iliyojengwa kwa msaada wa Serikali ya China imezinduliwa nchini Cambodia.Ujenzi wa gereji hiyo ambayo itatumika kurekebisha vifaa vya kijeshi ilianza kujengwa mwaka 2015. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Cambodia Jenerali...

REA kutoa mafunzo ya Nishati

NA FELISTA HENRY WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) wanatarajia kutoa mafunzo ya majuma mawili kwa mafundi na waendelezaji wa vyanzo vya umeme unaozalishwa kutokana na rasimali za nishati jadidifu. Serikali kupitia REA imeanza utekelezaji wa mradi kabambe wa awamu ya tatu wa...

Wednesday, February 15, 2017

Mfumko wa bei wapanda Misri, watalii wapungua

CAIRO, MISRI      Utalii nchini Misri umeshuka kutokana na thamani ya fedha kukosa thamani kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ajali ya ndege iliyotokea Oktoba 31, 2015 kwenye milima ya Sinai hivyo kukatisha safari za mashirika makubwa ya ndege. Takwimu...

Kim Jong-nam afariki dunia

KUALA LUMPUR, MALAYSIA Kim Jong-nam Aliyekuwa ndugu wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un ameuawa nchini Malyasia katika uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur. Maafisa wa Polisi nchini Malaysia wamesema kwamba Kim Jong Nam alishambuliwa juzi wakati alipokuwa akitarajia...

Tuesday, February 14, 2017

Vifo vya mapema India vyatisha

NEW DELHI, INDIA Uchafuzi wa hali ya hewa kutoka viwandani.                     UTAFITI wa kimataifa unaonyesha kuwa vifo vya mapema takribani milioni moja na laki moja nchini India vimetokea kutokana na uchafuzi wa...

Makonda ataja moja akabidhi majina 97 ya wanaojihusisha na dawa za kulevya

NA PENDO MICHAEL Gazeti la Habari Leo Februari 14, 2017 kuhusu Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kukabidhi majina 97 SIKU moja baada Rais John Magufuli kumwapisha Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga na kumtaka kusimamia kwa uadilifu mkubwa...