Thursday, March 2, 2017

Sober House Zanzibar kupekuliwa

NA SHARIFA SULEIMAN

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar   imezitaka  taasisi  husika kuzifanyia utafiti Soba House  zote ili kubaini kama zinajihusisha na kuingiza dawa za kulevya visiwani humo kinyume na malengo ya uanzishwaji wake.
Akizungumza katika kikao cha Baraza la Wawakilishi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa  Rais  Mohamed  Aboud amesema kuwa serikali haiwezi kuachia chombo ambacho chochote kinajihusisha na masuala ya dawa za kulevya ili kuwaponya vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa.
Nao baadhi ya wajumbe wa baraza hilo wameliomba Jeshi la Polisi kuwajibika ipasavyo ili wale wote wanajihusisha na biashara hiyo kuchukuliwa hatua   za haraka. 
Katika kikao  hicho wawakilishi wamepitisha maazimio mbalimbali ikiwamo viongozi na jamii kwa ujumla kushirikina katika kampeni ya kuwafichua watu wanaohusika na uingizaji wa dawa hizo.


0 Comments:

Post a Comment