Wednesday, March 15, 2017

Kortini kwa makosa ya mtandao

NA MWANDISHI WETU
Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam
Washtakiwa saba wa makosa ya Mtandao kutoka nchi za Pakistan na Sri lanka wamefikishwa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kujibu mashtaka saba yanayowakabili.

Wamesomewa mashtaka yao kwa mara ya kwanza ambapo hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo hivyo ushahidi utakapokamilia itasikilizwa mahakama kuu kitengo cha Wahujumu Uchumi.

Washtakiwa hao saba ni pamoja na sita kutoka Pakistan ambao ni Dilshad Ahmed, Rohail Yaqoob, Khalid Mahmood, Ashfaq Ahmad, Muhamad Aneess na Imtiaz Ahmad Qammar huku Ramesh Kandasamy akitokea Pakistan.

Mashtaka yao ni kuingiza vifaa vya mawasiliano bila kibali, kuunganisha vifaa vya mawasiliano kwenye mitandao ya nchi bila kibali, kuunganisha miundombinu ya mawasiliano nchini bila kibali, kutumia vifaa vya mawasiliano kuiba fedha kwa mtandao, kuendesha vifaa vya mawasiliano bila kibali, matumizi mabaya ya mitandao ya mawasiliano na kufanya kazi bila kibali cha kazi nchini.

Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Wahujumu Uchumi (mahakama ya mafisadi) ndio yenye uwezo wa kusikiliza kesi hii hivyo watuhumiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwani upelelezi ukikamilika kesi hiyo itasikilizwa mahakama kuu.


Kesi hii imewekwa kwenye kitengo cha uhujumu uchumi hivyo watuhumiwa wote wamerudishwa rumande mpaka watakapoomba dhamana Mahakama kuu kitengo cha Uhujumi Uchumi

0 Comments:

Post a Comment