Friday, March 10, 2017

TANESCO kuendesha operesheni 'Kata Umeme'

NA MWANDISHI WETU
Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) limetoa notisi ya siku 14 kwa wadaiwa wa Bili za Umeme na baada ya hapo wataendesha zoezi la ukataji wa umeme nchi nzima huku Wizara na Taasisi za Serikali zikidaiwa shilingi Bilioni 52,Makampuni  Binafsi na wateja wadogo shilingi Bilioni 94 pamoja na Shirika la Umeme Zanzibar(ZECO) shilingi Bilioni 127.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Dk. Tito Mwinuka alisema malimbikizo hayo ya madeni yamekuwa yakikwamisha jitihada za utekelezaji wa majukumu msingi ndani ya Shirika hilo, na kuongeza limekuwa likipitia wakati mgumu wakati Matengenezo ya miundombinu pamoja na utekeleza wa miradi mbalimbali.

Dkt. Mwinuka alisema zoezi hilo litakuwa endelevu kwa wadaiwa na watakoshindwa kulipa madeni na  hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wadaiwa hao.

Aidha Dkt. Mwinuka alisema iwapo wadaiwa hao watalipa malimbikizo ya madeni hayo Shirika litaweza kutatua kwa hatua baadhi ya changamoto ambazo zinawakabili.

Kwa muda mrefu Shirika la Umeme nchini limekuwa likilalamikia wateja wake kulimbikiza madeni na wanapoendesha zoezi la ukusanyaji wa madeni huwa hawafikii malengo.

0 Comments:

Post a Comment