Monday, March 13, 2017

Uzalishaji tumbaku washuka Chunya

NA MWANDISHI WETU
Shamba la Tumbaku nchini Tanzania
UZALISHAJI wa zao la Tumbaku kwa wakulima Wilaya ya Chunya (CHUTCU), mkoani Mbeya umeshuka katika misimu mitatu mfululizo kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuporomoka kwa bei ya zao hilo katika soko la dunia.
                  
Taarifa ya Chama Kikuu cha Ushirika wa zao la Tumbaku wilayani Chunya, imebainisha uzalishaji wa Tumbaku umeshuka kutoka Kilogramu Milioni 13.7 mwaka 2013/2014 mpaka kilogramu Milioni 11.4 zinazotarajiwa kuvunwa katika msimu huu.

Tumbaku likiwa ni miongoni mwa mazao makuu yanayoliingizia Taifa fedha za kigeni lakini likikosa ushindani mkubwa wa soko huria la wanunuzi ambao kwa sasa wapo wachache hapa nchini.

Hata hivyo wakulima wa tumbaku wilayani humo wameiomba Serikali kufanya mazungumzo na China ambayo inadaiwa kuwa na matumizi makubwa ya tumbaku kwa kununua asilimia 34 ya Tumbaku inayozalishwa Duniani lakini haijawahi kununua Tumbaku ya Tanzania.

Chama cha Ushirika wa Tumbaku wilayani Chunya, kina wanachama zaidi ya elfu nane wanaotoka katika vyama 23 vya msingi.


0 Comments:

Post a Comment