Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Mapambano dhidi ya Habari za Uongo hayapaswi kukoma

Habari za uongo, habari za uongo zinazosambazwa kwa lengo la kumdhuru mtu au jambo fulani, huifanya jamii kuwa na sintofahamu. Zinaweza kutumika kwa madhumuni ya kiitikadi, kisiasa au hata uhalifu, kama vile ulaghai mtandaoni unaolenga kuiba data ya kibinafsi.

Utandawazi na Athari zake katika Uandishi wa Habari

Katika jamii yetu ya kisasa, ambapo habari ziko kila mahali na zinaweza kupatikana kwa kila mtu, mara nyingi ni ngumu kutofautisha kati ya vyanzo vya kuaminika na habari bandia.

Uandishi wa Habari nguzo msingi mkuu kwa ujenzi wa jamii inayojitambua

JAIZMELA blog ni miongoni mwa vyanzo vya habari, zilizochakatwa kwa kuzingatia miiko ya uandishi wa habari.

Mila na Desturi ni nguzo muhimu

Mila na desturi ni nguzo muhimu sana katika utamaduni wa jamii yoyote ile; mila ni sawa na sheria zisizoandikwa. Mila ni taratibu za maisha na mwenendo zinazofuatwa na jamii fulani katika utendaji kulingana na historia na utamaduni wao. Mila zinatambulisha maadili ya jamii husika, huelezea namna jamii inavyoendesha mambo yake.

Tuesday, January 31, 2023

Mwalimu Nyerere: Shule ni Kiwanda au Shamba


 "Shule ni mahali pa kujifunza, hatutaki kubadili wazo hili, Haifai shule iwe kiwanda au shamba. Lakini lazima shule iwe kiwanda au shamba. Lakini ni lazima tuone kuwa kazi katika kiwanda cha shule au katika shamba la shule ni jambo la kawaida katika shughuli za kujifunza kuishi."

Saturday, January 28, 2023

Simba fans trust new appointed CEO Imani Kajula

 

Imani Kajula, new CEO of Simba SC

Trust is of utmost importance and an integral part of happy and fulfilling relationships, for both professional as well as personal relationships. 

Without trust, relationships are like a life without oxygen. You will feel suffocated and fail to maintain because one or both parties feel insecure or let down.

Lincoln Davenport Chafee is an American politician. He was mayor of Warwick, Rhode Island, from 1993 to 1999, a United States Senator from 1999 to 2007, and the 74th Governor of Rhode Island from 2011 to 2015.

Chafee said, “Trust is built with consistency.”



UWT Moshi vijijini yajitayarisha kujenga Chuo cha Ushonaji

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Moshi Vijini imekusudia kujenga Chuo cha Ushonaji ili kuwawezesha wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu ili waweze kujiimarisha kiuchumi. 

Hayo yalisemwa Januari 27,2023 na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Rwaichi Kaale kwenye mkutano  mkuu wa kwanza wa Baraza la Jumuiya hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa chama hicho Wilayani humo. 

Akizungumzia mpango kazi wa miaka mia Tano 2022-2027 Kaale amesema Jumuiya hiyo inakusudia kuwa na miradi ya kitegauchumi ili kuiwezesha Jumuiya hiyo kujiendeleza pasipo kutegemea wafadhili. 

Kaale aliitàja miradi hiyo ni pamoja na Chuo  cha ushonaji, kuanzisha kikundi cha mapishi, kuwa na mgahawa wa chakula na vinywaji pamoja na vyombo vya usafri kama vile bajaji. 

Katika hatua nyingine  Mwenyekiti wa UWT  Moshi Vijijini aliwaomba Wajumbe wa Baraza hilo kuvunja makundi na kuwataka kufanya kazi kwa pamoja ili kuendelea kuijenga Jumuiya hiyo na chama kwa ujumla. 

Kwa upande wake Katibu wa UWT Moshi Vijijini Shakila Singano, alisema katika kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa CCM  Jumuiya hiyo imeshiriki upandaji wa miti pamoja na kuwasajili wanachama wapya 500 kwa mfumo wa Kieletroniki ambapo matarajio ni kusajili wanachama 3,000 kwa mwaka 2023. 

Akifungua kikao hicho Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya Moshi Vijijini Ramadhan Mahanyu amesema Serikali ya awamu ya sita imeipatia Wilaya hiyo kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni mbili ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya chama. 

Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la UWT  Moshi Vijijini Gladness Mbwambo na Arapita Lyimo, wamesema uanzishwaji wa miradi ya kiuchumi ndani ya Jumuiya hiyo itaiwezesha UWT kuondokana na utegemezi sambamba na kuwasaidia vijana wa kike kujiepusha na ndoa za utotoni.




 

 

Polisi, DC Mwaipaya wafanya usafi kituo cha Afya Mwirange-Mwanga

 

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Watumishi wa kituo cha afya Mwirange, Januari 28,2023 wameshiriki zoezi la usafi wa mazingira katika baadhi ya maeneo yanayozunguka kituo hicho cha afya  ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mahusiano baina yao na wananchi ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu. 

Akizungumza mara baada ya zoezi la usafi Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Wilaya ya Mwanga (SSP) Hendry Nguvumali alisema, jeshi la polisi nchini lina kawaida ya kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi. 

SSP Nguvumali  alisema askari polisi wilaya ya Mwanga wameamua kuungana na wafanyakazi wa kituo cha afya Mwirange, ili kufanya usafi, lengo likiwa ni kuwa karibu na jamii pamoja na kutoa elimu kwa jamii itakayo lenga usalama wa Raia na mali zao, katika kuzuia na kupambana na uhalifu. 

Akishiriki zoezi la usafi Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Abdallah Mwaipaya alisema serikali wilayani humo imeungana na jeshi hilo katika kufanya usafi katika eneo ambalo linatoa huduma za afya kwa wananchi. 

Mwaipaya alisema maeneo ya kutolea huduma za afya yanapokuwa na mazingira salama yanasaidia kuepusha kuwepo kwa maambukizi mbalimbali ya magonjwa yasiyakuambukiza kwa wananchi wanaofika katika kupata huduma za kimatibabu. 

Alisema wilaya ya Mwanga inazo kata 20 na kati  ya hizo kata 16 zote zina polisi jamii na kwamba uwepo wa askari hao, umesaidia kupunguza changamoto za wananchi hao kusafiri kwenda katika kituo kikuu kupeleka mashauri mbalimbali. 

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mwirange Dkt. Yosya Foya, alisema kwenye kituo hicho wagonjwa wengi wanaofika kwa ajili ya kupatiwa matibabu wengi wao wanasumbuliwa na ugonjwa wa homa ya mapafu, kuharisha na malaria. 

Akizungumza Dkt. Afath Mohamed na Dkt. Joyce Kangero, walisema changamoto ya maradhi ambayo wakazi wa wilaya ya Mwanga wamekuwa wakiugua  na kuletwac katika kituo hicho cha afya yanaweza kuzuilika endapo watazingatia zaidi elimu ya afya ambayo imekuwa ikitolewa na wataalamu hao wa afya. 

Zoezi la usafi wa mazingira hufanyika kila Jumamosi ya mwisho wa kila mwezi ambapo Januari 28 mwaka huu Jeshi la Polis8i Mwanga kwa kusirikiana na uongozi wa serikali ya wilaya na uongozi wa kituo cha afya Mwirange wameshiriki kufanya usafi katika kituo hicho.





Tuesday, January 24, 2023

PICHA: Namna Chifu Mwariko alivyopumzishwa katika makaburi ya Manyema mjini Moshi







CHIFU ATHUMAN Omary MWARIKO “Mhelamwa” :Huyu ni yule aliomba noti ya Tanzania ichapishwe picha ya Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Magufuli, pia ndiye huyu aliomba mlima Kilimanjaro ufunikwe pazia, ndiye huyu aliandaa kinyago na kumpelekea Rais wa Urusi Vladmir Putin kwa ajili ya kufanikisha Kombe la Dunia 2018.


Chifu Mwariko is no more

 

Chifu Athuman Mwariko enzi za uhai wake

Mwili wa marehemu Chifu Mwariko ukiwa katika jeneza kuelekea makaburini Manyema, Moshi Mjini

Mkurugenzi  wa Taasisi ya Sanaa ya Kilimanjaro Cultural Heritage  Centre ya mkoani Kilimanjaro, Chifu Athuman Omari Mwariko amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79.

Taarifa za familia ya Chifu Mwariko zinasema alifariki dunia alfajiri ya Januari 22,2023 nyumbani kwake Maili Sita, na kuzikwa Jumatatu ya Januari 23,2023; saa 12 jioni.

Familia yake ilisema marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo ambapo siku chache kabla ya kifo chake alidai kuishiwa nguvu hadi umauti ukamkuta.

Chifu Mwariko aliwahi kufanya kazi na Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere pia Malkia Elizabeth II wa Uingereza.

Mwishoni mwa mwaka 2022 alimkabidhi Kifimbo Chifu Frank Marealle, mwenyekiti mstaafu wa Umoja wa Machifu Tanzania (UMT) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Mhandisi Zuberi Kidumo.

TAARIFA ZILIZOPITA  ZA CHIFU MWARIKO

BONYEZA LINKI HIZI

https://jaizmelanews.blogspot.com/2020/07/wizara-ya-fedha-yashauriwa-kuchapisha.html

https://jaizmelanews.blogspot.com/2020/11/mhelamwana-amkabidhi-kifimbo-mbunge.html

https://jaizmelanews.blogspot.com/2021/08/chifu-mwariko-ataka-chanjo-ya-uviko-19.html

https://jaizmelanews.blogspot.com/2022/06/kilimanjaro-cultural-heritage-centre.html

https://jaizmelanews.blogspot.com/2022/07/wasanii-wa-kilimanjaro-waishio-dar.html

https://jaizmelanews.blogspot.com/2022/10/chifu-marealle-akabidhi-madaraka-aonya.html

https://www.youtube.com/watch?v=8REybEtLY-4

https://www.facebook.com/johnson.jabir.735/videos/294583529107769

 

UVCCM Moshi Mjini yapanda miche 3,000

 

UVCCM Moshi Mjini wakiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mwenge katika zoezi la upandaji wa miti kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi.

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Wilaya ya Moshi Mjini  umewataka Vijana wa Jumuiya hiyo kusimamia misingi ya jumuiya hiyo kwani ndiyo nguzo kuu ya chama inayozalisha viongozi mbalimbali wa chama na Serikali. 

Akizungumza katika zoezi la upandaji miti ya matunda katika shule ya Msingi Mwenge iliyopo kata ya Kiusa Januari 24,2022 Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Sadath Sudi Ndibalema alisema UVCCM ni nguzo kuu inayopaswa kuzingatiwa katika mustakabali wa taifa hivyo vijana walioko ndani ya chama kuhakikisha kwamba wanaendelea kusimamia misingi hiyo.

Chama cha Mapinduzi kuliundwa Februari 5,1977 baada ya kuunganishwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha iliyokuwa Tanganyika, na Afro-Shiraz cha Zanzibar.

Azma ya zoezi la uoteshaji wa miche ya miti katika shule hiyo, Ndibalema alisema lengo ni kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi sambamba na wanafunzi kupata lishe ya wanafunzi hao.

Mkuu wa shule ya Msingi Mwenge Hellena John alisema, shule hiyo ilikuwa na uhitaji mkubwa wa miche ya miti ya matunda na kuipongeza Jumuiya ya Umoja wa Vijana kwakuweza kuwapatia miche hiyo.

Mkuu wa Shule ya Msingi Mwenge Bi. Hellen John

Katibu wa UVCCM Wilaya ya Moshi mjini Arafati Mbiruka alisema Jumuiya hiyo ya Vijana  wameamua kuotesha miti ya matunda katika shule ya msingi Mwenge ili kuboresha mazingira ya shule hiyo sanjari na wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo kupata matunda lishe ili kuboresha afya zao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kiusa, Khalid Shekoloa aliishukuru Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa UVCCM Manispaa ya Moshi kwa kuwezakupanda miti ya matunda katika shule hiyo kwani itakwenda kusaidia utatuzi wa changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi sanjari na kuwaomba wanafunzi wa shule hiyo kuendelea kuitunza 

Aidha Shekoloa amewataka kupanda miti kwa wingi itakayosaidia utunzaji wa mazingira ili kwenda sambamba na mpango wa Serikali wa upandaji miti ili kuzuia athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Sadath Ndibalema, mwenyekiti wa UVCCM Moshi Mjini

Naye Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Moshi Mjini kutoka kundi la Vijana  Ashiraf Baraka Malya, walisema bado kuna changamoto ya uelewa kwa jamii juu ya upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira.

“Upandaji miti ulioendeshwa na UVCCM Wilaya ya Moshi Mjini katika kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa CCM, itakwenda kuboresha mazingira ya shule huku akitoa wito kwa wanafunzi hao kuitunzana kuilinda ili kuwana mazingira yaliyo salama,”alisema Malya.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mwenge mjini Moshi wakiwa na miche ya miti

Zoezi la upandaji wa miti ni ikiwa ni maandalizi ya kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa CCM. Chama cha Mapinduzi kuliundwa Februari 5,1977 baada ya kuunganishwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha iliyokuwa Tanganyika, na Afro-Shiraz cha Zanzibar.

Stempu za Posta zikionyesha mambo mbalimbali ambayo Chama cha Mapinduzi iliyoyafanya ndani ya miaka 10 baada ya kuanzishwa kwake,ikiwamo Azimio la Arusha kutoka awamu ya kwanza na mwanzoni mwa awamu ya pili enzi za utawala wa Mwalimu Juliuys Kambarage Nyerere na Ali Hassan Mwinyi.




Wednesday, January 11, 2023

UVCCM Moshi Mjini yamjia juu Juma Raibu

 

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Moshi Mjini umemjia juu aliyetimuliwa Umeya wa Manispaa Juma Raibu kuacha kukikosoa chama chake hadharani hususani katika mitandao ya kijamii na badala yake kupeleka changamoto hizo kwa kufuata utaratibu wa chama.

Akizungumza  katika Kikao cha Kamati ya Utekelezaji ya CCM wilaya ya Moshi Mjini, Mwenyekiti wa  Sadath Sudi Ndibalemwa, alisema wako baadhi ya watu wachache ambao ni wana chama, baada ya kushindwa kuchaguliwa kwenye nafasi walizokuwa wameziomba kwenye chaguzi zilizomalizika hivi karibuni ndani ya chama hicho, wameunda kikundi cha kuanza kukichafua chama na viongozi wake  kwa kutumia mitandao ya kijamii.

Licha ya Ndibalemwa kutomtaja moja kwa moja Juma Raibu lakini mitandao ya kijamii ya aliyekuwa Meya wa Manispaa hiyo na Diwani wa kataya Bomambuzi  ameonyesha ukosoaji mkubwa wa chama hususani baada ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu kutangaza kuanza kwa mikutano ya hadhara kwa vyama vyote vya siasa nchini baada ya kuzuiwa enzi za utawala wa Dkt.John Pombe Magufuli.

Sadath Sudi Ndibalemwa,Mwenyekiti wa UVCCM wilaya wa Moshi Mjini

Katika akaunti ya Juma Raibu katika Instagram mnamo Januari 9,2023 aliandika, “Nemesikitishwa sana na baadhi viongozi wa chama changu mkoa na wachache wilaya na baadhi ya wanachama, kulaumu kuhusu Mh Rais Samia Kuruhusu mikutano ya hadhara, hakika huu ni udhaifu mkubwa sana na nikukimbia majukumu walioomba kwa Kuzoea kulala usingizi hakuna ushindi bila jasho…”

Juma Raibu anayefahamika kama ‘Man of the People’ yaani mtu wa Watu aliongeza katika utoaji wake wa maoni katika Instagram kuwa, “Twendeni kwa wananchi kusema yanayofanywa na CCM yetu na sio kuogopa mikutano tujipime kwa nguvu zetu Na sio kubebwa " hongera Mama Samia…tukutane Kazini”

Katika kuunga mkono juhudi zake Juma Raibu, wafuasi wake nao wameendelea kutoa maoni yao huku wakimtaka kukaza kamba zaidi

“Hao viongozi wa CCM wanaolalamika kwa nini mama karuhusu mikutano ingekuwa bora wangejiondoa kwenye nafasi zao, wawapishe watu wanaoweza kukisemea Chama. Viongozi dizaini hiyo ni wale waliozoea : " MSEREREKO " !!!!., Wana haja gani ya kuwa kwenye nafasi zao? waache uvivu walishazoea kulala usingizi. waamke...”alisema mfuasi aliyejitambulisha kwa jinala Job Faustine.

Viongozi wengine wa CCM waliojibu hoja za Juma Raibu ni Mrindoko Mwidadi ambaye ni Mwenyekiti wa Juumuiya ya Wazazi Tanzania mkoa wa Kilimanjaro alisema, “Viongozi gani wa Mkoa na Wilaya kwani tupo Mkoani?? pima maneno ya kuandika na kusema kwani ukiambiwa uthibitishe hili usije sema unaonewa!”

Kwa upande wake Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM (W) Moshi Mjini, Issa Bulilo alisema, “Hii sio sawa mkuu Viongozi wa Chama ngazi ya Mkoa na Wilaya wamelalamika wapi kufuatia Mh Rais kuruhusu mikutano??

Mnamo Januari 3,2023 Rais Samia aliruhusu mikutano ya vyama vya siasa baada ya marufuku ya miaka zaidi ya 6 iliyowekwa na mtangulizi wake, hayati John Magufuli.



Wednesday, December 21, 2022

Namna timu ya Taifa Morocco ilivyopokelewa mjini Rabat

Timu ya Taifa ya Morocco iliiweka Afrika katika ramani ya Dunia baada ya kushika nafasi ya tatu katika Kombe la Dunia 2022, ikitolewa na Ufaransa.

Hata hivyo iliambulia nafasi ya nne, ikizidiwa na Croatia iliyoshika nafasi ya tatu.





Conte amtaka Romero ndani ya saa 72 jijini London


Baba wa nyota wa Tottenham na timu ya taifa ya Argentina Victor Romero ameweka bayana kuwa kocha wa Spurs AntonioConte amemtaka nyota wake Cristian Romero kurudi London ndani ya saa 72 baada ya kusherekea ushindi wa Kombe la Dunia alilolitwaa  mnamo Desemba 18,2022.

Romero alicheza dakika zote 120 katika fainali dhidi ya Ufaransa wakilitwaa kwa mikwaju ya penati. Romero alikuwa kiungomuhimu katika kulitwaa kombe hilo akiwa na La Albiceleste.



Tuesday, December 20, 2022

MAKTABA YA JAIZMELA: Ifahamu Christmas

 

Tunaposema MERRY CHRISTMAS Maana yake ni FURAHA YA KUSANYIKO LA WAKRISTO.

Kwa hiyo hakuna mahusiano baina ya Christmas na kuzaliwa kwake Yesu Kristo Desemba 25. katika hili wala tusimung'unye maneno.

Nyakati zile Dola ya Rumi ilipokuwa ikitawala dunia walikuwa wana miungu yao ambayo iliabudiwa kila siku na Desemba 25 kila mwaka walifanya sherehe ya kuitukuza miungu yao hiyo.

MAJINA YA SIKU NA MIUNGU ILIYOABUDIWA

>Jumatatu (Monday) inatokana na moon day, kwa wapagani wa nyakati zile ilimaanisha siku ya kumwabudu mungu moon (mwezi).

>Jumanne (Tuesday) – inatokana na tiw’s day, kwa wapagani wa nyakati zile ilimaanisha ni siku ya mungu Tiw.

>Jumatano (Wednesday) – inatokana na wedn day au woden day, kwa wapagani ilimaanisha siku ya mungu wedn au woden.  

>Alhamisi (Thursday) - inatokana na ,,thor day,, kwa wapagani ilikuwa ni siku ya kumwabudu mungu thor.

 >Ijumaa (Friday) - inatokana na ,,frig day au freia day,, kwa wapagani ilikuwa ni siku ya

mungu frig au freia.  

>Jumamosi (Saturday) – inatokana na Saturn day (siku ya sayari zohari), kwa wapagani

ilikuwa ni siku ya kumwabudu mungu wa Kirumi aitwaye ,,Saturn,, yaani kwa Kiswahili

sayari ya zohari. 

>Jumapili (Sunday) –ilitokana na sun day (siku ya jua), kwa wapagani waKirumi ilikuwa ni

siku ya kumwabudu mungu sun (jua).


Kwa ujumla, Siku zote za juma, Warumi walizipa majina ya miungu yao, kwa sababu hao

kwa kipindi hicho ndiyo walikuwa watawala dunia kwa wakati huo. 

Katika miungu yote iliyotajwa hapo juu, mungu mkuu alikuwa ni mungu jua (sun) wao walimuita ni mungu asiye shindwa.

Hata baada ya utawala wa Dola ya Kirumi kuvunjika na nchi kuanza kujitawala bado watu kutoka mataifa mbalimbali waliendelea kuikumbuka miungu hiyo kila ifikapo Desemba 25 kila mwaka, na wengine walifunga safari kwena Mjini Rome Italia kushereheke sikukuu hizo za miungu ambazo hazikufahamika kwa jina la CHRISTMAS.

Hata warumi wenyewe waliposherehekea sikukuu hizo hawakuziona kuwa ni SIKUKUU ZA KIPAGANI maana walijiona wako sahihi (njia ya mtu ni njema machoni pake mwenyewe).

 CHRISTMAS.

Miaka ilivyozidikuendelea mbele ndipo baadhi ya watu waliopata kuifahamu kweli wakatambua hawakuwa sahihi kuendelea kuitumikia miungu ya kirumi wakati yupo Mungu muumba wa mbingu na nchi. Na hapo ndipo CHRISTMAS ilipoanzishwa. 

Lengo kuu la kuianzisha sikukuu ya christmas lilikuwa ni kuvunja nguvu au kufuta kabisa zile sherehe za kuiabudu au kuitukuza miungu ya kirumi kila Desemba 25 ya kila mwaka na ndio maana hata Christmas ilipoanzishwa ikapangwa katika tarehe sawa na sikuku ile ya kuiabudu miungu ya rumi.

Katika sherehe za Christmas watu walikuwa wakipokea zawadi kama vile nguo na vyakula nk, lakini katika zile sherehe za miungu ya ya warumi watu walikuwa wakiitolea zawadi ile miungu waliyoiabudu na huo ndio mwanzo wa Father Christmas. 

Hali hiyo iliwafanya watu kuanza kuyaendea makusanyiko yaliyopewa jina la Christmas na kusahau kuindea ile miungu yao kwa kuwa christmas ilitumika kwa matendo mema na ya faraja. 

Katika sherehe za Christmas watu walifundishwa matendo mema kwa kuwasaidia wahitaji kwa kuwapelekea zawadi kwa kunukuu maandiko kwamba hata Yesu Kristo alipozaliwa watu walipeleka zawadi zao. 

Hapo ndipo Christmas ilipoanza kuhusishwa na KUZALIWA KWA YESU KRISTO jambo ambalo ni kinyume na uhalisia wa maana ya jina au neno CHRISTMAS. 

Neno Christmas halipatikani popote katika biblia hata ukisoma kitabu cha MWANZO mpaka UFUNUO WA YOHANA huwezi kuliona neno Christmas. 

Pia huwezi kuizungumzia Christmas kwa maana ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo huku ukiwa umeshika Biblia mkononi kwa kuwa hakuna andiko litakalo kusapoti hoja zako. 

Kuamini CHRISTMAS ni kuzaliwa kwa Yesu Kristo huku ni kuamini kusiko sahihi.

 

KUZALIWA KWA YESU KRISTO. 

Biblia imekaa kimya kabisa kuhusiana na tarehe na mwezi na hata mwaka aliozaliwa Yesu Kristo, hata Yesu mwenyewe hakuwahi kuwaambia mitume na manabii wa nyakati zake kuhusiana na tarehe halisi ambayo yeye alizaliwa, na hata wanafunzi wake hawakuwahi kudadisi dadisi kuhusu jambo hilo. 

Hata kama mitume na manabii wa nyakati za Yesu wangepata kufahamu tarehe halisi aliyozaliwa Bwana Yesu, kuifahamu tarehe hiyo kusingeweza kuwa na msaada wowote katika maisha yao ya kiroho. 

Mtu yeyote anapokombolewa vitani baada yakuwa ameshikiliwa mateka kwa muda mlefu, atakachokifurahia mtu huyo ni tendo la kukombolewa kwake pomoja na jina la komandoo aliyemuokoa ili apate kushukuru kwa ujasiri wake, maana tarehe ya kuzaliwa kwa komandoo huyo wala hainamsaada kwake hata kama ataifahamu. 

LUKA 1:31, imeandikwa Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume, na jina lake utamwita jina lake Yesu. 

Huu ni ujumbe wa Malaika Gabrieli kwenda kwa Marimu na ilikuwa ni mwezi wa sita (6). 

Ujumbe unasema UTACHUKUA MIMBA, sio unachukua mimba. 

Maana kama ujumbe ungesema UNACHUKUA MIMBA, nayo ilikuwa ni mwezi wa sita, basi Yesu alifaa azaliwe mwezi wa tatu (sio wa kumi na mbili) hii ni kulingana na muda uaotakikana kwa mwanadamu kubeba mimba mpaka kuzaa mwana. 

Kwahiyo kwasababu ujumbe wa Malaika ulisema Tazama utachukua Mimba, hivyo haikuwekwa wazi kwamba hiyo mimba mariamu aliipata mwezi wa ngapi, maana ujumbe ni UTACHUKUA MIMBA na sio unachukua mimba. 

Hakuna mtume wala nabii yeyote aliyewahi kuikumbuka au kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo, hata Yesu mwenyewe hakuwahi kuagiza hayo.

MAFANIKIO YA KUANZISHWA KWA CHRISTMAS. 

Kama nilivyosema hapo awali kwamba, lengo la kuanzishwa kwa Christmas lilikuwa ni kuvunja na kuondoa kabisa zile sikukuu za kuabudu miungu ya kipagani ya kirumi, kwa kuianzisha christmas katika tarehe ileile ambayo wapagani wa kirumi waliitumia kuiabudu miungu yao, ndiomaana leo hii sherehe za kuiabudu miungu ya kirumi imebaki kuwa ni historia tu badala yake kila mtu anaifahamu Christmas kama ndio siku ya kuzaliwa Yesu Kristo (japo si kweli)

KDF yarahisisha mawasiliano Jeshi la Polisi


ACP Simon Maigwa 

Mwishoni mwa miaka ya 1970, mjasiriamali na mgunduzi wa mfumo wa simu za kiganjani nchini Marekani Martin Cooper alisema, “Tulijua kuwa watu hawapendi kuzungumza ndani ya magari, au  nyumba; au maofisini wanataka kuzungumza na watu wengine…Tulichokuwa tukiaminini kwamba namba ya simu inatakiwa kuwa ya mtu binafsi badala ya kuwepo eneo fulani.” 

Majaribio ya Cooper na wagunduzi wengine yameifanya dunia kwa sasa kuwa ya kipekee, mtu aweza kuwasiliana binafsi na mtu mwingine na wakazungumza ajenda zao za binafsi kwa wakati wowote. 

Hivyo ndivyo wadau wa maendeleo mkoani Kilimanjaro (KDF)  walivyoona fursa kupitia kampuni ya simu nchini Vodacom kwa namna gani wanaweza kurahisisha mawasiliano miongoni mwa Maofisa wa Jeshi la Polisi hivyo kuifanya kazi ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao kuwa nyepesi. 

Ilianzia hapa pale KDF ilipofanya makubaliano na Vodacom na kukubaliana nao kuwapa Polisi na wafanyakazi wote wa Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro namba za Vodacom ili waweze kuwasiliana wenyewe kwa wenyewe bure. 

Hatua hiyo inawafanya maofisa wa Polisi kupunguza gharama za mawasiliano miongoni mwao, kupitia mfumo wa Closed User Group (CUG) ambapo mfumo huo ni maalum kwa maofisa hao pekee. 

Tukio hilo la makabidhiano ya laini za simu limefanyika Desemba 19,2022 mjini Moshi katika ukumbi wa mikutano wa Kili Wonders. 

Kamanda wa Polisi Mkoani Kilimanjaro( ACP) Simon Maigwa amesema zoezi hili litaimarisha mawasiliano baina Askari na Askari katika utendaji wa kazi za Askari za kila siku. 

“Niwapongeze sana KDF kwa kuleta wazo hili ambalo limehusisha Kampuni ya Vodacom PLC,Chief Premium Beer, na Jeshi la Polisi.Ni hatua kubwa kwakweli na hili itarahisisha utendaji kazi kwa Askari wetu,Gharama hazitakuwepo hivyo mawasiliano yatafanyika kwa urahisi na kazi zetu pia zitaenda ukizingatia pia mawasiliano ni muhimu sana katika kazi zetu hizi,”    amesema  ACP Maigwa.

Aidha mjumbe wa KDF Rashid Tenga amesema zoezi hilo ni endelevu na halitadumu katika msimu huu wa sikukuu za mwishoni mwa mwaka. 

“Tutatoa Dk 300 za muda wa maongezi kwa shilingi Elfu mbili pekee mwezi mzima kwa askari wetu na zoezi hili ni endelevu, Iwapo kutakuwa na uhitaji zaidi wa huduma hii katika msimu wa sikukuu n.k tutaona namna ya kufanya,Hata hivyo tutaangalia pia uwezekano wa sekta nyingine kupatiwa huduma hii.,” 

“Tumeanza na wenzetu wa Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro na lengo kubwa ni kuhakikisha tunarahisisha mawasiliano na kufanya utendaji kazi wao kuwa rahisi zaidi.,mafanikio tutakayo yapata ndio yatasababisha tuangalie namna ya kuingia pia katika mikoa mingine,” ameongeza Tenga.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani Kilimanjaro akiwamo Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mjini Abbas Kayanda.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mjini Abbas Kayanda