Friday, July 19, 2024

New Lumumba Food Restaurant yazinduliwa mjini Moshi

 

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Zephania Sumaye akikata utepe katika uzinduzi wa New Lumumba Food Restaurant kwenye hafla iliyofanyika mjini Moshi mnamo Julai 19, 2024 katika viwanja vya Makao Makuu ya CCM Moshi Mjini; kutoka kushoto ni Katibu wa CCM Moshi Mjini Frida Kaaya, Mwenyekiti wa CCM Moshi Mjini Faraj Swai na Mkurugenzi wa mgahawa huo Athuman Ally Mfutu. (Picha na JAIZMELA/credited to: Jabir Johnson)

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeendelea kuwawezesha vijana kushiriki katika shughuli za ujasiriamali, ikiwemo kuwapatia fursa za kiuchumi hatua ambayo inadhihirisha ukuaji wa uchumi.

Hatua muhimu ya uzinduzi wa New Lumumba Restaurant, mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro chini ya mkurugenzi wake Athuman Ally Mfutu inadhihirisha namna CCM kinavyotoa fursa kwa vijana wake waliopo ndani ya chama hicho kuwekeza katika maeneo mbalimbali ikiwamo biashara.

New Lumumba Restaurant imeanza kwa kasi mpya baada ya uzinduzi wake wa nguvu ambao umetiwa chachu na viongozi wa chama hicho na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mjini Zephania Sumaye amekata utepe wa kuacha kwa utoaji wa huduma ya chakula na vinywaji wa mgahawa huo.

Akizungumza na wageni waalikwa wa hafla hiyo fupi mnamo Julai 19, 2024 katika viwanja vya Makao Makuu ya CCM Moshi Mjini DC Sumaye Mkuu amesema nia njema ya taifa kwa ujumla katika suala la maendeleondio chachu kubwa ya kuruhusu uwekezaji wa ndani pale wanapokidhi vigezo.

“CCM kwa nia njema kabisa yenye kuleta maendeleo ya nchi na watu wake imetoa fursa za uwekezaji kupitia chama hicho, ni vyema watu wakachangamkia fursa hizo ili waweze kukuza vipato vyao na hata kipato cha taifa kupitia kodi mbalimbali”, alisema DC Sumaye.


Aidha Mkuu huyo wa Wilaya, alimpongeza Mwekezaji aliyefungua Mgahawa huo Athuman Ally Mfutu, ambapo amesema Serikali itaendelea kushirikiana naye pamoja na wawekezaji wengine katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana Wilayani humo.


Akiongea katika hafla hiyo Naibu Mstahiki Meya Manispaa ya Moshi Stuwart Nathael, amesema uwekezaji huo utasaidia kukuza uchumi wa Manispaa ya Moshi kupitia njia mbalimbali kutokana na kukua kwa mzunguko wa fedha.


 “Tatizo kubwa katika nchi yetu ni ukosefu wa ajira, inapotokea kijana anaamua kuwa Mwekezaji Serikali itamuunga mkono kwa kuwa atachangia kukua kwa uchumi”, amesema Nathael.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Moshi Mjini Faraji Swai, amesema chama Wilayani humo, kitaendelea kushirikiana na Wawekezaji mbalimbali ili kuongeza fursa za uwekezaji Wilayani Moshi.


“Moja wapo ya yale yaliyomo ndani ya ilani ya CCM ni kwa serikali kutengeneza fursa za ajira; hili ndilo lililopelekea uongozi wa CCM wilaya kuja na wazo la kutafuta mwekezaji ambaye uwekezaji wake pia umebadilisha madhari ya ofisi kuwa nzuri”, amesema.


Awali akizungumza Mkurugenzi wa New Lumumba Food Restaurant Athuman Ally, amekishukuru Chama kwa kumpa ushirikiano katika uwekezaji alioufanya, ambapo amesema umetoa ajira kwa zaidi ya 15 wengi wao wakiwa ni vijana.



















 

0 Comments:

Post a Comment