Tuesday, September 10, 2024

Maandalizi maziko ya Askofu Chediel Sendoro yanaendelea

Askofu wa Dayosisi ya Mwanga ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Chediel Sendoro 

Maandalizi kwa ajili ya kumzika Askofu wa Askofu wa Dayosisi ya Mwanga ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Chediel Sendoro aliyefariki dunia kwa ajali usiku wa kuamkia Jumatatu ya Septemba 9, 2024

Ajali hiyo ilitokea eneo la Kisangiro, Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimaniaro, baada ya gari alilokuwa akiendesha Askofu Sendoro kugongana uso kwa uso la lori.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alikaririwa na Mwananchi kuwa ajali hiyo ilitokea leo saa 1:30 usiku, wakati gari lililokuwa likiendeshwa na Askofu huyo kutokea barabara ya Njiapanda ya Himo-Mwanga kuyapita magari mengine na kugongana uso kwa uso na lori aina ya Scania   lililokuwa likitokea Tanga -Arusha.


0 Comments:

Post a Comment