Bashasha, nderemo, na vifijo vimedhihirika kwa maelfu ya
wafuatiliaji wa siasa za ndani katika Tanzania baada ya kumuona Mwenyekiti wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu wakati akipandishwa
kizimbani kwa ajili ya kuendelea na kesi inayomkabili ya Uhaini.
Shangwe hizo zinaashiria mgawanyiko mkubwa wa kisiasa nchini,
ambapo siasa imegeuka kuwa jambo la hisia kali, na si la hoja. Badala ya
kuangalia uzito wa tuhuma na mchakato wa haki, baadhi ya watu wanaona haya ni
mafanikio ya kisiasa dhidi ya wapinzani wao.
Tundu Lissu alipandishwa kizimbani leo tarehe 19 Mei 2025
akitokea mahabusu anakoshikiliwa na vyombo vya usalama kutokana na mashtaka
yanayomkabili, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Tofauti na wakati wa kwanza leo katika viunga vya mahakama
hakukuwa na purukushani yoyote ya Jeshi la Polisi hatua ambayo imedhihirisha
kuwa Kama polisi wangekuwepo kwa wingi, hali hiyo ingeweza kufasiriwa kama
vitisho, hasa kwa wananchi waliokusanyika kwa amani na badala yake kunatoa
nafasi ya hali ya utulivu na ya ki-demokrasia kushamiri nchini.
Katika ukumbi wa mahakama Lissu alionekana kuzungumza maneno
mazito kuhusu mustakabali wa kesi hiyo hali akiendelea kusisitiza kuhusu
msimamo wa chama chake wa “No Reforms, No Election”.
Aidha baada ya kuendelea na mashtaka hayo Makamu Mwenyekiti
wa Chadema Joh Heche alipokelewa na mamia ya wafuasi wa chama hiyo.
Heche alisisitiza kuwa Lissu atarudi tena mahakamani hapo
mnamo tarehe pili ya Juni 2025 kuendelea na mashtaka hayo huku akisisitiza
baada ya kikao cha kamati ya utendaji wataendelea na mikutano ya “No Reforms,
No Election”.
Shangwe za wafuasi wa siasa dhidi ya mtu anayekabiliwa na
mashtaka mazito kama uhaini hazipaswi kuchukuliwa kuwa ni jambo la kawaida au
la kusherehekea. Badala yake, zinahitaji tafakari ya kina kuhusu mwenendo wa
siasa, hali ya demokrasia, na maadili ya taifa. Ni muhimu jamii itofautishe
kati ya ushindani wa kisiasa na kuunga mkono misingi ya haki, utu, na
demokrasia.
0 Comments:
Post a Comment