Monday, May 19, 2025

KESI YA TUNDU LISSU: Bashasha, Nderemo, Vifijo vyatawala Mahakama ya Kisutu

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu muda mchache kabla ya kesi kuanza mnamo tarehe 19 Mei 2025 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini  Dar es Salaam. (Picha na; MTANDAO)

Bashasha, nderemo, na vifijo vimedhihirika kwa maelfu ya wafuatiliaji wa siasa za ndani katika Tanzania baada ya kumuona Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu wakati akipandishwa kizimbani kwa ajili ya kuendelea na kesi inayomkabili ya Uhaini.

Shangwe hizo zinaashiria mgawanyiko mkubwa wa kisiasa nchini, ambapo siasa imegeuka kuwa jambo la hisia kali, na si la hoja. Badala ya kuangalia uzito wa tuhuma na mchakato wa haki, baadhi ya watu wanaona haya ni mafanikio ya kisiasa dhidi ya wapinzani wao.

Tundu Lissu alipandishwa kizimbani leo tarehe 19 Mei 2025 akitokea mahabusu anakoshikiliwa na vyombo vya usalama kutokana na mashtaka yanayomkabili, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Tofauti na wakati wa kwanza leo katika viunga vya mahakama hakukuwa na purukushani yoyote ya Jeshi la Polisi hatua ambayo imedhihirisha kuwa Kama polisi wangekuwepo kwa wingi, hali hiyo ingeweza kufasiriwa kama vitisho, hasa kwa wananchi waliokusanyika kwa amani na badala yake kunatoa nafasi ya hali ya utulivu na ya ki-demokrasia kushamiri nchini.

Katika ukumbi wa mahakama Lissu alionekana kuzungumza maneno mazito kuhusu mustakabali wa kesi hiyo hali akiendelea kusisitiza kuhusu msimamo wa chama chake wa “No Reforms, No Election”.

Aidha baada ya kuendelea na mashtaka hayo Makamu Mwenyekiti wa Chadema Joh Heche alipokelewa na mamia ya wafuasi wa chama hiyo.

Heche alisisitiza kuwa Lissu atarudi tena mahakamani hapo mnamo tarehe pili ya Juni 2025 kuendelea na mashtaka hayo huku akisisitiza baada ya kikao cha kamati ya utendaji wataendelea na mikutano ya “No Reforms, No Election”.

Shangwe za wafuasi wa siasa dhidi ya mtu anayekabiliwa na mashtaka mazito kama uhaini hazipaswi kuchukuliwa kuwa ni jambo la kawaida au la kusherehekea. Badala yake, zinahitaji tafakari ya kina kuhusu mwenendo wa siasa, hali ya demokrasia, na maadili ya taifa. Ni muhimu jamii itofautishe kati ya ushindani wa kisiasa na kuunga mkono misingi ya haki, utu, na demokrasia.

Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment