Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Mapambano dhidi ya Habari za Uongo hayapaswi kukoma

Habari za uongo, habari za uongo zinazosambazwa kwa lengo la kumdhuru mtu au jambo fulani, huifanya jamii kuwa na sintofahamu. Zinaweza kutumika kwa madhumuni ya kiitikadi, kisiasa au hata uhalifu, kama vile ulaghai mtandaoni unaolenga kuiba data ya kibinafsi.

Utandawazi na Athari zake katika Uandishi wa Habari

Katika jamii yetu ya kisasa, ambapo habari ziko kila mahali na zinaweza kupatikana kwa kila mtu, mara nyingi ni ngumu kutofautisha kati ya vyanzo vya kuaminika na habari bandia.

Uandishi wa Habari nguzo msingi mkuu kwa ujenzi wa jamii inayojitambua

JAIZMELA blog ni miongoni mwa vyanzo vya habari, zilizochakatwa kwa kuzingatia miiko ya uandishi wa habari.

Mila na Desturi ni nguzo muhimu

Mila na desturi ni nguzo muhimu sana katika utamaduni wa jamii yoyote ile; mila ni sawa na sheria zisizoandikwa. Mila ni taratibu za maisha na mwenendo zinazofuatwa na jamii fulani katika utendaji kulingana na historia na utamaduni wao. Mila zinatambulisha maadili ya jamii husika, huelezea namna jamii inavyoendesha mambo yake.

Tuesday, February 4, 2025

Bweni la wanafunzi Kaloleni Islamic Seminary laungua moto

Chumba cha tatu cha Bweni la Makka katika shule ya Kaloleni Islamic Smeinary baada ya kuzimwa kwa moto. Picha na Jabir Johnson/JAIZMELA correspondent

Zaidi ya wanafunzi 50 wa kike, Shule ya Sekondari ya Kaloleni Islamic ya mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wamenusurika kuungua na moto baada ya bwenì walilokuwa wakiishi kulipuka moto leo saa saba mchana.

Taarifa za wafanyakazi na majirani wa karibu na shule hiyo ndio waliofanikisha ujio wa haraka wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambalo lilifika katika eneo la tukio na kufanikiwa kuzima moto katika bweni hilo la wasichana lenye vyumba 20.

Wakiwa katika huzuni kuu kutokana na viaa vyao kuungua moto, Wanafunzi wa kike shuleni hapo walipata fursa ya kuzungumza na waandishi wa habari waliofika katika eneo hilo ambapo lamic

Chanzo cha moto huo kinaelezwa kuwa ni wanafunzi wa chumba cha tatu ndani ya bweni kilicholipuka moto kuwa na vifaa vinavyolipuka.

Akizungumza na vyombo vya habari katika eneo la tukio Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jeremiah Mkomagi amesema hakuna majeruhi yaliyojitokeza licha ya vifaa vya wanafunzi yakiwamo madaftari, magodoro.

“Majira ya saa 7 na dakika 17 mchana tulipata taarifa za tukio la moto katika shule hii kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kwa jina la Urio, kikosi kilichokuwepo zamu kilifika na kusaidiana na wafanyakazi na majirani kuzima moto,” alisema Mkomagi.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo Mohammed Hussein Migeto amesema wakati tukio la moto linajitokeza alikuwa nje ya shule na alirudi haraka na kuchukua hatua stahiki kuhakikisha wanafunzi wapo salama licha ya wawili miongoni mwao kupata mshtuko na kukimbizwa hospitalini.

“Wanafunzi wawili walipata mshtuko baada ya kusikia kelele za moto kutokana kwa wanafunzi wenzao wakati wakiwa msikitini,…” aliongeza Mwalimu Migeto.

Hii ni mara ya pili kwa shule hiyo ya Kiislamu kupatwa na janga la moto; Moto katika shule unaweza kuwa na athari kubwa kwa jamii nzima; Jamii inaweza kukosa huduma muhimu za elimu kwa wanafunzi ambao wanashindwa kurudi shule kwa sababu ya uharibifu unaojitokeza wakati wa majanga ya moto.









Saturday, February 1, 2025

Watatu wafariki dunia papo hapo kwa ajali mjini Moshi

 

Watu watatu wamefariki dunia kutokana na ajali iliyohusisha gari dogo na mabasi mawili ya Abiria mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, kwa kile kinasadikika ni mwendokasi na kuovertake.

Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro lilifika eneo la Kaanan, mjini hapa ilipotokea ajali hiyo kwa ajili ya uokoaji ambapo gari aina ya Toyota Rav 4 yenye namba za usajili T 592 EKU iligongana uso kwa uso na basi la Esta Luxury Coach tana na changamoto hiyo katika barabara ya Moshi- Arusha ikitokea Himo.

Mashuhuda wa tukio hilo wanasema mabasi ya abiria ya Kidia na Esta Luxury Coach ndio chanzo cha ajali hiyo baada ya Kidia kushindwa kumaliza kulipita gari la Esta ambapo Rav 4 ilikutana uso kwa uso na basi la Esta.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Godfrey Mzava amesema ajali hiyo ilitokea leo saa 12:30 asubuhi na kwamba abiria waliokuwepo katika basi la Esta walipatiwa basi jingine kuendelea na safari ya Dar es Salaam.

Miili ya Marehemu iliyokuwemo katika Rav 4 imehifadhiwa katika Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya KCMC kwa ajili ya uchunguzi zaidi na taratibu nyingine za mazishi.



Thursday, January 30, 2025

MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN 2025: Kushindwa kuandika Wosia kumetajwa chanzo cha migogoro ya ardhi na mirathi

Wakili Boniface Mwabukusi
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)

Kushindwa kuandika wosia kumetajwa kama chanzo cha migogoro ya ardhi na mirathi

Akizungumza katika uzinduzi wa wiki ya sheria mnamo Januari 29, 2025 mkoani Kilimanjaro Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) Wakili Boniface Mwabukusi alisema Migogoro ya ardhi na mirathi ni matatizo yanayoweza kutokea kutokana na sababu mbalimbali, na mara nyingi husababishwa na mifumo ya kijamii, kiuchumi, na kisheria.

“Huduma ya Msaada wa kisheria ni ibada, ni ibada kwasababu tunashughulika na maisha ya watu ya kila siku; ni wakati wa kuifanya kwa unyenyekevu na ukamilifu wake na kuelewa kwamba hata mitume wangekuwepo leo au Yesu angekuwa Kilimanjaro sehemu ya kwanza kufika ingekuwa hapa kwenye Legal Aid,” alianza Mwabukusi

Aidha Mwabukusi alisema kuwa kutokuwa na utaratibu mzuri katika kugawa mali za marehemu, kunakosababishwa na maelezo hafifu ya wosia, au kutokuwepo kwa wosia kabisa.

“Matatizo mwakubwa na changamoto ya legal yanayogusa wananchi yapo kwenye ardhi na mirathi, na yanachangiwa na utafsiri mbaya wa sheria au watu wakorofi tu na kwenye mirathi ni kwasababu hatupendi kuandika wosia,” alisisitiza Mwabukusi.

Mwabukusi aliongeza kuwa wakati mwingine, wanajamii wanachukulia kwamba wao wanastahili sehemu fulani ya ardhi au mali ya familia, na hivyo kuleta migogoro kuhusu nani anapaswa kumiliki nini.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu alithibitisha kuwepo kwa changamoto ya ardhi katika mkoa wake huku akitaja sababu ya ongezeko la watu na ardhi kuwa finyu.

“ Tuseme ukweli waliotanguliwa wanasema mkoa wa Kilimanjaro liko tatizo kubwa la ardhi....ni kweli....kwasababu ardhi yetu ni finyu; na ardhi hiyo ilishagawanywa kwa muda mrefu na waliokuwa nayo; na watu wanaongezeka na wazazi wanaendelea kuzaa, ili wagawane vihamba ndipo tatizo linapoanzia; ” alisema Babu.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro amesema wananchi wanapoitafuta haki wanaonyesha ustaarabu na ndio sababu ya kufanyika kwa kampeni ya utoaji wa msaada wa kisheria nchini iliyoratibiwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Watu hawa wanajitokeza kwa wingi katika kampeni hii ya Mama Samia Legal Aid kwasababu wanaitafuta haki ili wakidhi kiu yao; ya kupata haki, Ukiona wananchi wanaitafuta  haki kwanza ni kuwapongeza sana kwasababu wananchi hao wamestaarabika; tunakwenda kuhakikisha Mama Samia Legal Aid inaleta Haki ambayo italiinua taifa,” alisema Dkt. Ndumbaro.

Kauli mbiu mwaka huu katika wiki na siku ya Sheria, “ Tanzania ya 2050; Nafasi ya Taasisi zinazosimamia Haki Madai katika kufikia Malengo Makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo.”

 







Monday, January 27, 2025

Yuji ‘Gump’ Suzuki awasili Cape Town (SA) kwa mguu, baada ya siku 210

Yuji "Gump" Suzuki mnamo Januari 26, 2025 jijini Cape Town baada ya kuwasili akihitimisha safari yake ya kilometa 6,000 kutoka Nairobi, Kenya. Yuji alitumia miezi saba kutoka Juni 2024 hadi Januari 26, 2025.


“Hayo ni Maisha Yangu”; alisikika Mjapan mmoja akitamka mnamo Januari 26, 2025 katika viunga vya jiji la Cape Town nchini Afrika Kusini baada ya kuwasili akitokea Nairobi, Kenya kwa mguu.

Cha kustaajabisha ni kwamba Mjapan huyo aliyefahamika kwa jina la Yuji ‘Gump’ Suzuki aliwasili katika jiji hilo lililo umbali wa kilometa 6,400 kutoka Nairobi, Kenya akiwa na mkokoteni wa matairi mawili akiongozana na vijana wengine wawili wa Kijapan.

Mjapan Yuji mwenye umri wa miaka 34 aliwasili jijini Cape Town humo akitumia siku 210 sawa na takribani miezi saba tangu alipoianza safari yake mnamo Julai 2024, alipita nchini Tanzania, Zambia, Zimbabwe na Namibia kabla ya kuingia Afrika Kusini.

Mapema asubuhi ya Januari 26, 2025 akiwa na mkokoteni wake uliojizolea umaarufu mkubwa wa ‘Rickshaw’ wenye uzito wa kilogramu 100; Yuji aliukokota kwa furaha na kuwapongeza vijana wenzake kwa kumuunga mkono katika safari hizo za kitalii

Nisingeweza kufanya bila ninyi ndugu zangu, ninatembea kwa furaha, nimekuwa nikisafiri kwa miaka tisa sasa na nimekuwa nikiungwa mkono nanyi hivyo narudisha kwenu. Hayo ni maisha yangu,” alisema Suzuki.

Yuji aliongeza kuwa changamoto za barabarani kubwa lakini iliyokuwa ngumu zaidi ni ya kupenya Jangwa la Namibia.

Kwa mujibu wa tovuti yake; mnamo mwaka 2016-2017 Yuji Suzuki; alitembea kutoka China hadi India pia kilometa 2,500 alizunguka barani Ulaya mnamo mwaka 2017; pia kilometa 5,100 nchini Marekani kati yam waka 2022-2023.

Mkokoteni wa magurudumu mawili (Rickshaw) ulianza kutumika lini?

Rickshaw ya kwanza ilivumbuliwa nchini Ufaransa mwishoni mwa karne ya 17; kwa ajili ya mahitaji ya usafiri licha ya uwepo wa aina nyingine za vyombo vya usafiri. Miaka hiyo ya 1679 Ufaransa ilikuwa imeendelea sana katika masuala ya usafiri  aina ya “Omnibus” ambazo zilikuwa zinafanana na waendeshaji wa mikokoteni ya kuuza mvinyo katika mitaa ya jiji la Paris. Wakati huo mikokoteni hiyo ilikuwa ikisukumwa na watu wawili mmoja anakuwa mbele akivuta na mwingine nyuma akisukuma. Huyu wa mbele alikuwa akishikilia mbao fulani ikiwa ni sehemu ya kutafuta mizania na kuongoza uelekeo anaoutaka.

Wasanii wa uchoraji hawakuwa nyuma Msanii Claude Gillot alichora picha yake aliyoipa jina la “Les deux carosses” ambao ulionyesha mikokoteni hiyo miwili; mchoro huo aliuchora mnamo mwaka 1707.

Katika ardhi ya Japan, wao walivumbua kivyao mnamo mwaka 1869 ambapo kipindi cha utawala wa Tokugawa (1603-1868) kulipigwa marufuku ya matumizi ya vyombo vya usafiri vinavyotumia matairi ikiwamo mikokoteni. Wakati mikokoteni ya Rickshaw ikianza ndio kipindi ambacho Japan ilikuwa imeanza kukua katika masuala ya ufundi.

Izumi Yosuke anasalia kuwa mvumbuzi wa kwanza wa Rickshaw nchini Japan akishirikiana na Suzuki Tokujiro na Takayama Kosuke ambao wote kwa pamoja walipata wazo kutokana na namna magari ya Farasi yanavyofanya kazi, miaka michache baadaye waliyaingiza mitaani na kuwa sehemu ya maisha kisha kusambaa hadi China na kwingineko.

Credit to: Jabir Johnson/ JAIZMELA/Mashirika ya Habari/Wikipedia 

+255 693 710 200






 

Thursday, January 23, 2025

Tundu Lissu ni nani?

 

Tundu Antipas Lissu
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

Tundu Lissu ni mwanasheria maarufu nchini Tanzania, na aliwahi kuwa Rais wa chama cha wanasheria Tanganyika(TLS), mwaka 2020 aligombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema na kushindwa na mgombea wa chama tawala John Magufuli, aliyefariki dunia Machi 2021. 

Lissu aliyenusurika kifo Septemba 2017 baada ya kushambuliwa kwa risasi mjini Dodoma, ni maarufu kwa siasa za mapambano na ''ulimi mkali'' hali ambayo mara imemuweka katika mabishano makali na wanasiasa wezake hususan wa chama tawala. Amekuwa akisema alipopigwa risasi alikuwa ''nusu mfu'' 

Kuanzia mwaka 2010 Lissu alikuwa mbunge wa Singida Mashariki na alijipatia umaarufu kwa michango yake bungeni hususan ya kuikosoa serikali ya Rais Jakaya Kikwete na baadaye Hayati Rais John Pombe Magufuli.

Lissu ni msomi wa kiwango cha shahada ya umahiri aliyoipata nchini Uingereza katika Chuo Kikuu cha Warwick kati ya mwaka 1995 na1996. Kabla ya hapo alipata shahada ya kwanza ya sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikohitimu mwaka 1994. 

Maisha yake yamekuwa zaidi katika harakati za kutetea haki za binadamu na kutoa msaada wa kisheria kwa watu wenye mahitaji lakini wana uwezo mdogo wa kifedha. Aliwahi pia kuwa mwenyekiti wa chama wanasheria za Mazingira Tanzania (LIT) katika miaka ya 1990.

Sunday, January 5, 2025

China Communication Construction Company kuanza ujenzi barabara ya Ndungu-Mkomazi

 

Wakala wa barabara Nchini (TANROADS) wametakiwa kuhakikisha wanatoa kipaumbele kwa wazawa kwenye miradi ya ujenzi barabara na kuwawezesha vijana kupata ajira kwa lengo la kuinua uchumi wa wananchi .

Waziri wa ujenzi Abdalla Ulega ametoa agizo hilo alipokuwa Wilayani Same mkoani Kilimanjaro katika hafla ya kumkabidhi mkandarasi CHINA COMMUNICATION CONSTRUCTION COMPANY (CCCC) mradi wa ujenzi wa barabara ya Ndungu -Mkomazi yenye urefu wa kilomita 36 itakayo tengenezwa kwa kiwango Cha lami ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa serikali kuhakikisha Uwepo wa Maendeleo na ufanisi katika sekta ya usafiri na usafirishaji.

Ulega amesema ujenzi wa barabara hiyo utaondoa kero ya usafiri pia kuimarisha na kuchochea Kasi ya uchumi ,kilimo, biashara na utalii hususani kwa wananchi wote wa wilaya ya Same, Kanda ya kaskazini na Pwani.

"Serikali imetoa fedha zaidi ya bilioni 59 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii ya Ndungu -Mkomazi itakayowakomboa wananchi kiuchumi hivyo vijana changamkieni fursa za ajira zitakazotokana na ujenzi wa barabara hii,zalisheni kwa wingi Mpunga,Tanga wizi na ndizi ili kukuza mtandao wa biashara Kati ya Same ,Mikoa ya Tanga na Pwani" amesema Waziri Ulega.

Kutokana na umuhimu mkubwa wa ujenzi wa barabara hiyo utakao rahisisha huduma ya usafiri na usafirishaji amesisitiza vijana wa maeneo yanayopitiwa na mradi wa ujenzi kuchangamkia fursa za ajira zitokanazo na mradi huo.

Awali Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro amesema ujenzi wa barabara hiyo inayopita kwenye idadi kubwa ya wananchi Wilayani humo utarahisisha Maisha na kuibua fursa nyingi za kiuchumi .

Barabara ya Ndungu- Mkomazi ni Moja ya barabara muhimu hapa nchini hususani katika shughuli za Maendeleo zinazochochea uchumi wa nchi kupitia kilimo,utalii na biashara na kwa kuliona hilo serikali imeshakamilisha malipo ya awali takribani bilioni 5.8 kwa mkandarasi ili kuanza kazi rasmi ya ujenzi wa kilomita 36 kwa kiwango Cha lami.

Credit to: Elizabeth Mkumbo; Freelancer/JAIZMELA




Saturday, December 28, 2024

Mambo 7 muhimu Ushiriki wa Viongozi wa Siasa; Mwanga Marathon & Festival 2024

 

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Kilimanjaro Seleman Mfinanga mnamo Desemba 27, 2024 baada ya kumaliza kukimbia Kilometa 10 katika Mwanga Marathon & Festival 2024. Tukio hilo la riadha ni la kwanza kubwa kufanyika katika wilaya ya Mwanga ambayo kwa sasa inaongozwa na Bi. Mwanahamisi Munkunda akiwa ni mwanamke wa pili kushikilia wadhifa wa ukuu wa wilaya ya Mwanga tangu ilipoanzishwa katikati ya miaka ya 1970. (Picha na Kija Elias/Jabir Johnson; JAIZMELA News.)

MWANGA, KILIMANJARO

Hatimaye mnamo Desemba 27, 2024 Mwanga Marathon & Festival  imefanyika kwa mara ya kwanza katika viunga vya wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro ambako kumeshuhudiwa watu mbalimbali wakiwamo viongozi wa siasa wakishiriki mbio hizo zilizowakutanisha zaidi ya watu 500.

Miongoni mwa wanasiasa walioshiriki mbio hizo ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Kilimanjaro Seleman Mfinanga. Wengine ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Lameck Michael Mlacha, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Karia Rajabu Magaro, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mwanga  Mwl. Ibrahim Mnzava, Mbunge wa Jimbo la Mwanga Wakili Joseph Anania Tadayo, Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Mwanahamisi Munkunda, Mkuu wa Wilaya ya Rombo Mwl. Raymond Mwangwala, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Japhari Kubecha na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Simon Maigwa.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza mbio za Kilometa 10; Mfinanga alitoa shukrani zake za dhati kwa Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bi. Mwanahamis Munkunda kwa kuthubutu kuanzisha wazo hilo la kila mwishoni mwa mwaka.

Kwa upande wake Bi. Munkunda alisema, Tamasha ambalo ni la msimu wa kwanza kufanyika wilayani humo, litatumika kama njia kuwafungulia milango ya fursa katika sekta ya utalii ambayo kwa sasa inaitangaza nchi vizuri pamoja na kutoa ajira kwa wingi.

“Wilaya ya Mwanga imejaliwa kuwa na vivutio vingi ya kihistoria na mandhari nzuri, ambazo ni fursa kwa wana Mwanga, niwaombe wananchi kuvitumia fursa hii, kwa ajili ya kuongeza kipato na kuifungua wilaya yetu.”alisema DC Munkunda.

Katika uchambuzi wa leo, tutaangazia namna viongozi wa kisiasa wanaposhiriki shughuli za michezo wanavyotoa athari chanya katika jamii wanayoiongoza.

1. Taswira ya Uongozi wa Kijamii na Usawa

  • Kujali Afya ya Jamii: Viongozi wanapoonyesha kujihusisha na michezo, wanatoa ujumbe kwamba wanathamini afya ya wananchi na wanatambua umuhimu wa michezo katika kuboresha ustawi wa jamii. Hii inaweza kuwa na athari nzuri katika kuhamasisha watu, hasa vijana, kushiriki katika shughuli za kimaisha zinazoleta manufaa kwa afya.
  • Promosheni ya Usawa: Viongozi wanaweza kuonyesha mfano wa ushirikiano na mshikamano katika michezo, bila kujali tofauti za kisiasa, kijinsia, au kabila. Hii inaweza kuimarisha umoja na kujenga taswira ya usawa na mshikamano katika jamii.

2. Taswira ya Uhusiano na Watu

  • Kujitolea kwa Jamii: Viongozi wanaposhiriki katika michezo, wanaonyesha kwamba wao pia ni sehemu ya jamii na wanajali shughuli zinazohusu raia wa kawaida. Hii inaweza kusaidia kuvunja vikwazo vya kisiasa na kuimarisha uhusiano wao na wananchi.
  • Kufikia Kila Mtu: Kwa kushiriki katika michezo ya uma, viongozi wanaweza kuonyesha kuwa wako karibu na wananchi na wanajali maslahi ya kila mtu, sio tu ya watawala wa juu.

3. Taswira ya Kukuza Picha ya Kiongozi "Mwenye Afya"

  • Kiongozi Mwenye nguvu na afya bora: Viongozi wanaoshiriki katika michezo kama riadha au soka wanaweza kujenga picha ya kuwa na afya bora, nguvu na uwezo wa kukabiliana na changamoto za kisiasa. Hii inaweza kuwa na manufaa katika kutengeneza picha ya kiongozi mwenye nguvu na uwezo wa kuhimili shinikizo la kazi.
  • Mfano wa Kuigwa: Viongozi wanaweza kuwa mfano wa kuigwa katika shughuli za afya na ustawi, na hivyo kuhamasisha watu kutunza miili yao na kuwa na tabia njema za kiafya.

4. Taswira ya Kukuza Umoja na Mshikamano

  • Mshikamano wa Kitaifa: Viongozi wanaoshiriki katika michezo wanapata nafasi ya kuonyesha mshikamano na umoja wa kitaifa. Hii ni muhimu hasa katika nchi zenye changamoto za kisiasa au kijamii, ambapo michezo inaweza kuwa njia ya kuunganisha watu kutoka makundi mbalimbali.
  • Tafakari ya Kawaida ya Kijamii: Shughuli za michezo ni mojawapo ya maeneo ambayo mara nyingi huleta watu pamoja bila kujali hali zao za kisiasa, hivyo viongozi wanaposhiriki, wanatuma ujumbe wa ushirikiano na ufahamu wa umoja wa kitaifa.

5. Taswira ya Kubuni Fursa za Uchumi na Maendeleo

  • Kuonyesha Mchango wa Michezo katika Uchumi: Viongozi wanaposhiriki katika michezo, wanaweza pia kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya michezo na burudani. Hii inaweza kusaidia kukuza utalii, ajira na maendeleo ya miundombinu ya michezo.
  • Kukuza Talanta na Vipaji: Viongozi wanaweza kuhamasisha vijana kuwa na nidhamu, kujitolea na kuonyesha kwamba michezo inaweza kuwa njia ya kujijengea maisha bora, iwe ni kwa njia ya ajira au mafanikio ya kitaifa.

6. Taswira ya Kupunguza Mizozo na Kuimarisha Amani

  • Michezo Kama Kigezo cha Amani: Viongozi wanaoshiriki katika michezo, hasa katika matukio ya kitaifa au kimataifa, wanaweza kutumia nafasi hiyo kuhamasisha amani, mshikamano, na kupunguza mizozo. Michezo inaweza kuwa na athari nzuri katika kuleta watu pamoja na kupunguza mivutano ya kisiasa au kijamii.

7. Taswira ya Kutojali Hali Halisi ya Kisiasa

  • Hatari ya Kupuuza Masuala ya Kisiasa: Ingawa kushiriki michezoni kunaweza kuwa na athari nzuri, baadhi ya watu wanaweza kuona kama ni juhudi za kiongozi kupuuza masuala ya kisiasa na kujaribu kujipatia umaarufu kwa njia isiyokuwa na maana. Viongozi wanaweza kuonekana kuwa wanajali michezo zaidi kuliko masuala ya kijamii au kisiasa yanayohitaji haraka kutatuliwa.
  • Kujionyesha kwa Manufaa ya Kisiasa: Ikiwa viongozi wanashiriki katika michezo kwa lengo la kujinufaisha kisiasa, jamii inaweza kuona kama ni mbinu ya kutafuta umaarufu au kupunguza shinikizo la kisiasa kwa njia isiyozungumzia masuala ya msingi.

Hitimisho:

Viongozi wa kisiasa wanapojihusisha na michezo, wanatoa taswira ya uongozi wa kijamii, umoja, na afya, lakini pia wanaweza kujikuta wakikabiliwa na changamoto za kutafsiriwa vibaya ikiwa michango yao itakuwa ya kisiasa zaidi kuliko ya dhati. Jambo muhimu ni kuhakikisha kuwa ushiriki wao ni wa kweli na unalenga kuleta manufaa kwa jamii nzima, si tu kwa kujipatia umaarufu.

Makala haya yameandaliwa na Jabir Johnson; Mwandishi wa Habari, Kilimanjaro +255 693 710 200 Baruapepe: jabirjohnson2020@gmail.com





 

Tuesday, December 24, 2024

AMEC Kilimanjaro yawatoa hofu waumini kuhusu uhuru wa kuabudu

Mkuu wa Jimbo la Kilimanjaro wa Kanisa la Africa Mission Evangelism (AMEC) Mchungaji Wilson Kawiche amewataka waumini wanaojiunga na kanisa hilo kutambua kuwa Katiba ya Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania inawalinda kwa uamuzi wao wa kufuata Imani ya dini wanayoitaka kuitumikia.

Akizungumza katika Hafla ya kumsimika Mchungaji Paul Assey wa AMEC Usharika wa Kileo, wilayani Mwanga iliyofanyika mnamo Desemba 22, 2024 Mchungaji Kawiche alisema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua uhuru wa mtu kuabudu Imani ya dini anayotaka bila kikwazo chochote.

Mchungaji Kawiche alisema haki hiyo inapatikana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hasa katika Ibara ya 19, ambayo inasema kwamba kila mtu ana haki ya kuwa na uhuru wa kutafuta, kupokea na kutoa maoni na habari, pamoja na uhuru wa kuamini na kutekeleza dini au imani anayotaka, bila kujali dini, kabila, au hali nyingine yoyote ya kibinafsi.

Aidha Mkuu huyo wa Jimbo la AMEC Kilimanjaro aliyasema hayo wakati akitoa nasaha kwa waumini walioamua kurudi kuhudumu na kanisa hilo  ambapo Mchungaji Kawiche aliwatoa hofu kuhusu uamuzi wao wa kumrudia Mungu wao.

Waliorudi hemani mwa Bwana walitoa shukrani zao za dhati kwa kanisa la AMEC Kileo kuwapokea na kuwafanya wapya tena ndani ya Yesu Kristo.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Furaha Tanzania Mchungaji Jones Mollah aliyealikwa kwenye hafla hiyo ya kumsimika Mchungaji Assey aliwata waumini hao waliorudi kundi kutambua kuwa walikuja kwa miguu yao wenyewe na kwamba wasitishwe na hila za adui shetani kwamba hawatafanikiwa hemani mwa Bwana.

Katika hafla hiyo Mchungaji Assey alikula kiapo cha kulitumia Kanisa la AMEC Kileo kwa uaminifu wote na kulihudumia kusanyiko la watu wa Mungu

Askofu Mkuu wa AMEC Tanzania Mchungaji Baltazar Kaaya alimsimika Mchungaji Assey kwa sheria za kanisa hilo ambapo hafla hiyo ilisindikizwa na Uimbaji kutoka kwaya ya Mtiini Mungu ya AMEC Ulshoro mkoani Arusha.

Kwa ujumla, uhuru wa imani nchini Tanzania ni haki muhimu inayotambuliwa na Katiba na sheria, na inalinda haki ya kila mtu kuamini na kutekeleza imani yake kwa huru, ingawa kwa baadhi ya nyakati, kuna mipaka ili kulinda utawala wa sheria na haki za wengine.

AMEC inaundwa na takribani makusanyiko 100 ya Wakristo wa Kilutheri katika eneo la Kaskazini mwa Tanzania. Limesambaa zaidi katika eneo la chini ya Mlima Meru mkoani Arusha na sasa linaendelea kuongezeka kuzunguka Mlima Kilimanjaro na tambarare kuelekea Upareni.

Credit to: Jabir Johnson, +255 693 710 200 jabirjohnson2020@gmail.com

AMEC Tanzania yamwingiza kazini Mchungaji Paul Assey

Kanisa la Africa Mission Evangelism (AMEC) limemsimika rasmi Paul Assey kuwa mchungaji wa Usharika wa Kileo, jimbo la Kilimanjaro katika hafla iliyofanyika katika usharika wa Kileo wilayani Mwanga.

Hafla hiyo ya kumsimika Mchungaji Assey ilifanywa na Askofu Mkuu wa AMEC Tanzania Baltazar Kaaya ilienda sambamba na Ibada ya Jumapili na Uimbaji kutoka kwaya ya Mtiini Mungu  AMEC-Ulshoro ya Arusha.

Mkuu wa Jimbo la Kilimanjaro Mchungaji Wilson Kawiche alikuwa miongoni mwa watumishi wa Mungu walioongoza ibada hiyo ambayo iliwaleta pamoja Wakristo wa madhehebu hayo nchini

Hafla hiyo ilianza kwa utaratibu wa kanisa, kuwasimika watumishi wake ambapo Wachungaji mbalimbali wa kanisa hilo, walimzunguka Mchungaji Assey na kuanza kusoma Neno la Mungu mmoja baada ya mwingine.

Hatua iliyofuata ilikuwa ni kukiri kwa kinywa chake, kiapo cha kulitumikia Kanisa la Mungu kwa uaminifu wote hata ukamilifu wa dahali.

Mchungaji Assey na viongozi wakuu wa Kanisa hilo akiwamo Askofu Mkuu wa AMEC Tanzania Baltazar Kaaya walisaini kiapo hicho muhimu tayari kwa kuanza rasmi kazi ya Mungu katika Parokia ya Kileo.

Awali akizungumza kabla ya hafla ya kumwingiza kazini Mchungaji Assey, Mchungaji Judah kutoka Amec Arusha alisema ni furaha kuu ku

Katika ibada hiyo Mchungaji Judah alipata nafasi ya kutoa neon la Mungu kwa waliohudhuria ibada hiyo wakiwamo ndugu jamaa na marafiki.

Aidha ujumbe kutoka Kanisa la Furaha Tanzania ukiongozwa na Askofu Jones Mollah ulitolewa katika ibada hiyo

Katika hafla hiyo ulienda sanjari na kuwarudisha hemani mwa Bwana waumini walioamua kurudi tena kumtumikia Mungu katika kanisa hilo.

Nasaha zilitolewa kwa waliorudi hemani mwaka Bwana huku wakisisitizwa kuvumilia hila za Shetani za kutaka kuwarudisha nyuma.

Aidha Mkuu wa Jimbo la Arusha Mchungaji Elidaima Mushi alitoa nasaha kwa Mama Mchungaji Assey namna ya kumtunza Mchungaji Assey ili aweze kuifanya kazi ya Mungu kwa ukamilifu wote,

Ndugu, Jamaa na Marafiki walipata fursa ya kutoa shukrani zao kwa tukio hilo muhimu katika maisha yao, ambapo Kaka wa Mchungaji Assey alitoa shukrani za dhati kwa niaba ya kundi hilo.

Kuwasimika wachungaji kuanza kazi ya Mungu ni kitendo cha kanisa kumtambulisha na kumwezesha mchungaji kuingia katika jukumu rasmi la kuongoza na kutunza kundi la waumini. Hii ni hatua muhimu katika huduma ya kiroho  ambapo mchungaji anapewa mamlaka na wajibu wa kuhubiri Neno la Mungu, kuongoza ibada, kufanya huduma za kiroho kama vile ubatizo, ndoa na mazishi na  pia kutunza na kulinda mwanzo wa Imani ya waumini.

AMEC inaundwa na takribani makusanyiko 100 ya Wakristo wa Kilutheri katika eneo la Kaskazini mwa Tanzania. Limesambaa zaidi katika eneo la chini ya Mlima Meru mkoani Arusha na sasa linaendelea kuongezeka kuzunguka Mlima Kilimanjaro na tambarare kuelekea Upareni.

 

Credit to: Jabir Johnson, +255 693 710 200 jabirjohnson2020@gmail.com






Sunday, December 15, 2024

Mangi Gilbert Gilead Shangali Asimikwa Isaleni, Wari-Machame; Kilimanjaro

Mangi Gilbert Gileadi Shangali akiinua ngao kwa mkono wa kulia ikimaanisha ulinzi wa jamii ya Kimachame, mkono wa kushoto akiwa na mkuki baada ya kusimikwa na Chifu Frank Marealle (wa kwanza kushoto) lililofanyika Isaleni, Wari-Machame wilayani Hai mkoani Kilimanjaro mnamo Desemba 14, 2025. (Picha na Jabir Johnson/JAIZMELA News)

Shauku Kubwa waliyokuwa nayo Wamachame ya kumsimika Mangi wa 52 wa jamii hiyo imetimizwa baada ya Mangi Gilbert Gilead Shangali kusimikwa rasmi kuiongoza jamii hiyo baada ya miongo mitano ya kusubiri hafla hiyo.

Mwenyekiti wa Machifu nchini Tanzania Frank Marealle ndiyo aliyeongoza hafla ya kumsimika Mangi Gilbert Shangali iliyofanyika katika eneo la Isaleni, Wari-Machame wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.

Tukio hilo la lililokuwa na mvuto wa aina yake kulishuhudiwa viongozi wa serikali, dini na wanasiasa mbalimbali wakihudhuria hafla hiyo ambayo ilionyesha utamaduni halisi wa jamii hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo ambayo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu alikuwa mgeni rasmi, Mkufunzi wa Chuo Kishiriki cha KCMC Tumaini University Harold Shangali alisema mchango wa Rais Samia Suluhu Hassa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  aliyepewa na machifu jina laChifu Hangaya ni mkubwa katika kuendeleza utamaduni wa Mtanzania.

Chifu Marealle alimpaka mafuta ya Simba, Mangi Gilbert Shangali pia alimvika vazi la ngozi ya Chui kisha kumkalisha katika kiti cha asili cha Umangi wa Machame, huku wazee wengine wa koo za Kimachame walimkabidhi mkuki na usinga.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu alimkabidhi Mangi Gilbert Shangali chombo cha asili cha kuweka chakula ikiwa ni ishara ya utoshelevu katika masuala ya lishe kwa Wamachame.

Hafla hiyo ilisindikizwa na unywaji wa Supu, mbege na nyama choma ya ng’ombe na mbuzi. Takribani ng’ombe 10 zilichinjwa kwa ajili ya kumsimika Mangi Gilbert Shangali.

Mbali na uwepo wa watu mbalimbali, jamii ya wanyamwezi wa Tabora, wahangaza kutoka magharibi mwa ziwa Victoria, Wamasai kutoka Arusha na Manyara walihudhuria hafla hiyo kuonyesha umoja na mshikamano wa kiutamaduni wa Kitanzania unaoundwa na jamii 123.

Kwa upande wao Rebeka Matayo Ndalishao alisema hafla ya kumsimika Mangi Gilbert Shangali linawakumbusha kuwa utamaduni wa Wamachame wa kuwa na kiongozi thabiti anayesimamia maadili na mwenendo mzima wa jamii hiyo.

Yunisi Munisi anaanza kwa kuimba Kimachame akielezea wito wa jamii kutunza mazingira na maadili ya jamii yao.

Simbo Jacob Salema anasema Mangi katika jamii ya Kimachame walikuwa na kazi kubwa ya kulinda jamii na kutunza maadili.

Mangi katika jamii ya Wachagga ni viongozi wa jamii na mara nyingi huwa na jukumu la kusimamia amani, utulivu, na utawala katika jamii zao. Wanatoa maamuzi ya kisheria na kijamii kuhusu migogoro, urithi, ndoa, na haki za jamii. Pia Mangi huhakikisha kuwa tamaduni za asili hazipotei na kwamba vizazi vipya wanajua na kuenzi urithi wao.

Utamaduni na maisha ya watu wanavyoishi Machame kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya uongozi wa Mangi. Aliruhusu dini ya Ukiristo iingie Machame. Alilazimisha watu wa Machame kwenda kukamata ardhi sehemu za tambarare, aliruhusu shule zianzishwe, n.k

Credit to: Jabir Johnson, +255 693 710 200



Wahitimu 3,246 watunukiwa shahada mbalimbali Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi

Wakati, Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), kikifikisha umri wa miaka 10 tangu kupewa ithibati ya kuwa chuo kikuu kamili, Spika mstaafu wa Bunge, Anne Makinda, amewatunuku kwa mara ya kwanza wahitimu 3,246 shahada mbalimbali.

Kati ya wahitimu hao wa fani mbalimbali, wamo wanataaluma sita waliotunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD).

Idadi hiyo ya wahitimu inazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka, tangu Makinda aliporithi mikoba ya aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Mtendaji wa kwanza wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Pius Msekwa na Msaidizi wa karibu wa Hayati, Mwalimu Julius Nyerere.

Akizungumza Novemba 13, 2024 katika mahafali ya 10 ya chuo hicho, Mwenyekiti wa Baraza la chuo hicho, George Yambesi, amemweleza Makinda kuwa, kati ya wahitimu hao, atawatunuku astashahada, stashahada, shahada za awali, stashada za uzamili, shahada za umahiri na shahada ya uzamivu.

Wanataaluma waliotunukiwa Shahada hiyo ya PhD, ni pamoja na Dkt. Alex Nyagango, Mtawa Dkt. Bernadette Temba, Dkt. Emmanuel Mkilia, Dkt. George Budotela, Dkt. Julieth Koshuma na Dkt. Pamela Liana.

Naye, Makamu Mkuu wa Chuo hicho cha MoCU, Prof. Alfred Sife, alimweleza Spika mstaafu Makinda, wanazuoni hao na wahitimu wengine, ni alama tosha ya mafanikio ya kujivunia katika maisha yao, kwani inatokana na juhudi na maarifa waliyowekeza.

Credit to: Elizabeth Mkumbo, Freelancer; Jaizmela News



Monday, December 9, 2024

Usuli kuhusu Wamachame

Wamachame ni moja ya makabila ya asili ya Tanzania, hasa linapopatikana katika Mkoa wa Kilimanjaro. Wamachame ni kundi la watu wanaozungumza lugha ya Kichaga cha Kimachame, ambayo ni sehemu ya familia ya lugha za Kibantu. Hawa ni miongoni mwa jamii za kiasili za Kilimanjaro, na wengi wao wanaishi katika mkoa huo, hasa katika maeneo ya milimani na sehemu za tambarare.

Wamachame wanatokea katika maeneo ya milimani ya mkoa wa Kilimanjaro, na wamejulikana kwa kufanya shughuli za kilimo cha mazao kama vile mahindi, viazi, mpunga, na matunda. Historia ya Wamachame inahusiana sana na milima ya Kilimanjaro, ambapo wengi wao ni wakulima na wafugaji. Wamachame ni mojawapo ya makabila ya Tanzania yanayotajwa kuwa na uhusiano na jamii za maeneo ya milimani na makabila mengine ya karibu kama Wazaramo, Watu wa Pare, na Wachaga.

Utamaduni wa Wamachame ni wa kipekee na umejikita sana katika mila na desturi zao za jadi. Hawa ni watu ambao wanahusisha sana familia na jamii katika shughuli za kijamii. Msingi wa maisha yao ni kilimo cha mazao mbalimbali, na pia wanajihusisha na shughuli za ufugaji na biashara ndogo ndogo.

Kama vile makabila mengine ya mkoa wa Kilimanjaro, Wamachame wamekuwa na uhusiano wa karibu na Wazaramo, Wachaga, na Wapare, ambao pia wanafanya shughuli za kilimo na biashara. Watu wa kabila hili wanajivunia sana utamaduni wao na mila zao.

Dini ya Wamachame ni mchanganyiko wa imani za jadi na dini za kisasa kama Ukristo na Uislamu. Wengi wao ni Wakristo, lakini bado kuna sehemu za jamii ambazo zinaendeleza imani zao za jadi.

Wamachame wana mfumo wa familia na jamii inayozingatia mshikamano na ushirikiano. Kuna mifumo ya uongozi wa kijamii na wazee wa jamii wanaohusika na masuala ya kijamii na kimila. Katika baadhi ya maeneo, viongozi wa jadi bado wanaheshimika na kusaidia katika kutatua migogoro na masuala ya kijamii.

Kwa kumalizia, kabila la Wamachame ni jamii ya watu wenye utajiri wa urithi wa kijasiri na tamaduni za kipekee, na wao ni sehemu muhimu ya jamii ya Kilimanjaro na Tanzania kwa ujumla.