Tuesday, April 15, 2025

MMFA yapokea marekebisho ya Uwanja wa Railway Moshi; Meya Kidumo apewa maua yake

 

Marekebisho ya Uwanja wa Railway uliopo Njoro katika Kata ya Njoro, Manispaa ya Moshi ukifanyiwa marekebishwa kwa makatapira ikiwa ni mwendelezo wa kuinua vipaji vya soka kwa kuboresha miundombinu ikiwamo maeneo ya kuchezea yaani pitch. Meya wa Manispaa ya Moshi Injinia Zuberi Kidumo ndiye Diwani wa Kata hiyo ambako Uwanja wa Railway unafanyiwa marekebisho. (Credit to: Jabir Johnson/JAIZMELA).

Chama Cha Soka Manispaa ya Moshi (MMFA) mkoani Kilimanjaro kimepokea kwa shangwe kuu marekebisho yanayoendelea ya Uwanja wa Soka wa Railway.

Hatua ya kufanya marekebisho ya uwanja vya soka wa Railway yanatoa taswira kadhaa muhimu kuhusu maendeleo ya michezo, usimamizi wa miundombinu, na mwelekeo wa kijamii na kiuchumi katika mji.

Akizungumza uwanjani hapo Katibu wa MMFA Mwalimu Japhet Mpande amesema marekebisho yanaonyesha dhamira ya Manispaa ya Moshi kuboresha mazingira ya michezo kwa vijana na wakazi wake.

Mwalimu Mpande amesema yote yanaonesha kuwa Moshi inajitahidi kufikia viwango bora vya michezo na kuvutia mashindano ya kitaifa, pia inaweza kusaidia vijana wengi kujiingiza katika michezo kitaaluma au kupata ajira kupitia michezo.

………

Aidha Mwalimu Mpande ameongeza kuwa marekebisho ya viwanja mara nyingi huambatana na mpangilio mzuri wa mazingira ambapo yataongeza mvuto wa Manispaa ya Moshi kama sehemu inayojali mazingira na ustawi wa jamii.

Kwa upande wao wakazi wa Njoro uliopo uwanja wa Railway wamepokea kwa furaha na kutoa pongezi lukuki kwa Meya wa Manispaa ya Moshi Injinia Zuberi Kidumo ambaye ni Diwani wa Kata ya Njoro.

Aidha wakazi hao wameapa kuulinda uwanja huo ikiwamo tabia mbaya za udokozi, pia watu kukatisha uwanjani ili uendelee kuwa lulu kwa kata ya Njoro na Manispaa ya Moshi kwa ujumla.

…………….

Gharama za ukarabati huo bado hazijawekwa wazi mpaka utakapokamilika na taarifa rasmi kutolewa.

Viwanja bora vinaweza kuleta fursa za biashara ndogondogo (mfano wauzaji wa vyakula, vinywaji, mavazi ya michezo) na kuongeza mapato ya halmashauri kupitia kodi na matumizi ya viwanja kwa shughuli mbalimbali.

Uwanja wa Railway unafanyiwa marekebisho ikiwa ni takribani miongo minne kupita licha ya kwamba umekuwa ukitumiwa katika mashindano mbalimbali ikiwamo Zuberi Cup.















Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment