Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Tuesday, October 25, 2016

Kizimbani kwa wizi wa magodoro Aga Khan

NA JABIR JOHNSON WATU wawili wamepandishwa kortini katika mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam kujibu mashtaka kwa kosa la wizi wa vitu mbalimbali vya Hospitali ya Aga Khan yakiwamo magodoro 20. Wakisomewa mashtaka yao jana na Mwendesha Mashtaka Grace Mwanga mbele...

Kizimbani kwa kubaka

ILALA, DAR ES SALAAM MKAZI wa Majohe Plaza jijini Dar es Salaam Ally Ramadhani (23) amepandishwa kizimbani kwa kosa la kumbaka msichana wa miaka 17. Akisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Flora Mjaya, mwendesha mashtaka Ashura Mnzava alidai Mei 5 mwaka huu eneo la Kinyerezi mshtakiwa...

Monday, October 24, 2016

Dk. Mashinji Oktoba 23

Alichokisema Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk.Vincent Mashinji baada ya uchaguzi wa meya wa Kinondoni, Oktoba 23, 2016 kuhusu kufungua kesi mahakamani. “Chadema hakitakuwa chama cha kulalamika…hatutakuwa walalamishi tena tutakusanya ushahidi…Hii...

Sunday, October 23, 2016

Sita kortini kwa unyang’anyi

NA MWANDISHI WETU WATU sita wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha. Mbele ya Hakimu Mkazi John Msafiri, Mwendesha Mashtaka Sylivia Mitanto alidai Ramadhani Athumani (18), Jabil Muhando (17), Khalifan Humba (16), Nurdin Muhando (17), Abdul Omary (15) na Hamad Mohamed...

Friday, October 21, 2016

Dereva wa daladala jela miaka 7

ILALA, DAR ES SALAAM MAHAKAMA ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam imemhukumu dereva wa daladala mkazi wa Ubungo wa External Mohamed Amir Ramadhani kwa wizi wa Sh. 6,700,000. Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Catherine Kiyoja alisema ushahidi wa mahakama umethibitisha...

Thursday, October 20, 2016

‘Scorpion’ afunguliwa upya mashtaka, abadilishiwa hakimu

NA JABIR JOHNSON Salum Njewete 'Scorpion' akitolewa nje ya ukumbi wa mahakama ya Wilaya ya Ilalajijini Dar es Salaam jana chini ya ulinzi mkali baada ya kusomewa mashtaka upya. MSHTAKIWA wa kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha Salum Njwete (34) ‘Scorpion’  amefutiwa...

Wednesday, October 19, 2016

‘Panya Road’ afufuka mochwari

TEMEKE, DAR ES SALAAM  MKAZI wa Buza wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Isaack Ernest (16), miongoni mwa wahalifu wa kundi la ‘Panya Road’ amefufuka katika Chumba cha Kuhifadhi Maiti cha Hospitali ya Temeke siku chache baada ya kufikishwa hapo kama maiti. Tukio hilo...

‘Scorpion’ kupandishwa korti leo

NA MWANDISHI WETU Salum Njewete MSHTAKIWA wa unyang’anyi wa kutumia silaha Salum Njwete (34) maarufu Scorpion anatarajiwa kupandishwa tena katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam leo. Scorpion anapandishwa kortini kwa mara ya tatu baada ya kesi yake kuahirishwa...

Tuesday, October 18, 2016

Jela miaka 30 kwa kubaka mlemavu

ILALA, DAR ES SALAAM MAHAKAMA ya Wilaya Ilala jijini hapa imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela mkazi wa Pugu Bangulo Mathayo Mtanga (20) kwa kosa la kumbaka binti wa miaka 14. Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Florah Haule alisema kesi hiyo ilifika mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Julai 21, 2015 na mshtakiwa alitenda kosa hilo Mei 28, 2015...

Monday, October 17, 2016

Shahidi wa tukio la wizi Tabata Bima asimulia

ILALA, DAR ES SALAAM SHAHIDI namba moja wa tukio la unyang’anyi wa kutumia silaha lililotokea Tabata Bima jijini Dar es Salaam Antimi Kimati ameiambia Mahakama ya Wilaya ya Ilala kuwa alimwona mtuhumiwa namba moja Amir Mohamed ‘Songambele’ akiwa na bunduki siku ya tukio. Kesi...

Thursday, October 13, 2016

Dk. Didas Masaburi is no more

CHANIKA, DAR ES SALAAM Meya wa zamani wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi amefikwa na umauti jana majira ya saa tatu na nusu usiku katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa. Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na ndugu yake, Dk. Makongoro Mahanga...

Muuza maji jela kwa kuiba mti

NA MWANDISHI WETU MAHAKAMA ya Mwanzo ya Ilala imemhukumu Muuza maji mkazi wa Keko jijini Dar es Salaam Emmanuel Issa (38) kifungo cha miezi minane jela kwa kosa la kuiba miti 12 aina ya mchikichi. Akisoma hukumu hiyo Hakimu Asha Mpunga alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo...

Wednesday, October 12, 2016

Miaka 30 jela kwa unyang’anyi

NA MWANDISHI WETU MKAZI wa Kinondoni kwa Manyanya Stephano Focus ‘ Malenga Tyson’ (29) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini hapa baada ya kukiri kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha. Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Adelf Sachore...

Monday, October 10, 2016

HUKUMU YA AJABU; Ahukumiwa kifungo cha maisha mara mbili na miaka 14

Washtakiwa wa kesi ya kulawiti, wizi na kusambaza picha za udhalilishaji Erick Mdemu (mbele) na Juma Richard (katikati) wakitoka katika mahakama ya Wilaya ya Ilala chini ya ulinzi mkali baada ya kuhukumiwa kwenda jela.  NA JABIR JOHNSON MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala...

Friday, October 7, 2016

‘Scorpion’ mtoboa macho kizimbani

NA JABIR JOHNSON Salum Njewete 'Scorpion' akipelekwa katika karandinga la Jeshi la Magereza baada ya kesi yake kuahirishwa kutokana na upelelezi kutokamilika.  MWALIMU wa sanaa za mapigano Salum Njewete (34) maarufu Scorpion na mkazi wa Yombo Machimbo amepandishwa...