
Tuesday, October 25, 2016
Kizimbani kwa wizi wa magodoro Aga Khan

NA JABIR JOHNSON
WATU wawili wamepandishwa kortini katika mahakama ya Wilaya ya
Ilala jijini Dar es Salaam kujibu mashtaka kwa kosa la wizi wa vitu mbalimbali
vya Hospitali ya Aga Khan yakiwamo magodoro 20.
Wakisomewa mashtaka yao jana na Mwendesha Mashtaka Grace Mwanga
mbele...
Kizimbani kwa kubaka

ILALA, DAR ES
SALAAM
MKAZI wa Majohe Plaza jijini Dar es Salaam Ally Ramadhani
(23) amepandishwa kizimbani kwa kosa la kumbaka msichana wa miaka 17.
Akisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Flora Mjaya,
mwendesha mashtaka Ashura Mnzava alidai Mei 5 mwaka huu eneo la Kinyerezi
mshtakiwa...
Monday, October 24, 2016
Dk. Mashinji Oktoba 23

Alichokisema Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Dk.Vincent Mashinji baada ya uchaguzi wa meya wa Kinondoni,
Oktoba 23, 2016 kuhusu kufungua kesi mahakamani.
“Chadema hakitakuwa
chama cha kulalamika…hatutakuwa walalamishi tena tutakusanya ushahidi…Hii...
Sunday, October 23, 2016
Sita kortini kwa unyang’anyi
NA MWANDISHI WETU
WATU sita wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya
Ilala jijini Dar es Salaam kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha.
Mbele ya Hakimu Mkazi John Msafiri, Mwendesha Mashtaka
Sylivia Mitanto alidai Ramadhani Athumani (18), Jabil Muhando (17), Khalifan
Humba (16), Nurdin Muhando (17), Abdul Omary (15) na Hamad Mohamed...
Friday, October 21, 2016
Dereva wa daladala jela miaka 7

ILALA, DAR ES SALAAM
MAHAKAMA ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam imemhukumu dereva wa
daladala mkazi wa Ubungo wa External Mohamed Amir Ramadhani kwa wizi wa Sh.
6,700,000.
Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Catherine Kiyoja alisema ushahidi
wa mahakama umethibitisha...
Thursday, October 20, 2016
‘Scorpion’ afunguliwa upya mashtaka, abadilishiwa hakimu
NA
JABIR JOHNSON
Salum Njewete 'Scorpion' akitolewa nje ya ukumbi wa mahakama ya Wilaya ya Ilalajijini Dar es Salaam jana chini ya ulinzi mkali baada ya kusomewa mashtaka upya.
MSHTAKIWA
wa kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha Salum Njwete (34) ‘Scorpion’ amefutiwa...
Wednesday, October 19, 2016
‘Panya Road’ afufuka mochwari

TEMEKE, DAR ES
SALAAM
MKAZI wa Buza wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Isaack
Ernest (16), miongoni mwa wahalifu wa kundi la ‘Panya Road’ amefufuka katika
Chumba cha Kuhifadhi Maiti cha Hospitali ya Temeke siku chache baada ya
kufikishwa hapo kama maiti.
Tukio hilo...
‘Scorpion’ kupandishwa korti leo

NA MWANDISHI WETU
Salum Njewete
MSHTAKIWA wa unyang’anyi wa kutumia silaha Salum Njwete (34) maarufu
Scorpion anatarajiwa kupandishwa tena katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini
Dar es Salaam leo.
Scorpion anapandishwa kortini kwa mara ya tatu baada ya kesi yake
kuahirishwa...
Tuesday, October 18, 2016
Jela miaka 30 kwa kubaka mlemavu
ILALA, DAR ES SALAAM
MAHAKAMA ya Wilaya Ilala jijini hapa imemhukumu kifungo cha miaka 30
jela mkazi wa Pugu Bangulo Mathayo Mtanga (20) kwa kosa la kumbaka binti wa
miaka 14.
Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Florah Haule alisema kesi hiyo
ilifika mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Julai 21, 2015 na mshtakiwa alitenda
kosa hilo Mei 28, 2015...
Monday, October 17, 2016
Shahidi wa tukio la wizi Tabata Bima asimulia

ILALA, DAR ES SALAAM
SHAHIDI namba moja wa tukio la unyang’anyi wa kutumia silaha
lililotokea Tabata Bima jijini Dar es Salaam Antimi Kimati ameiambia Mahakama ya
Wilaya ya Ilala kuwa alimwona mtuhumiwa namba moja Amir Mohamed ‘Songambele’
akiwa na bunduki siku ya tukio.
Kesi...
Thursday, October 13, 2016
Dk. Didas Masaburi is no more

CHANIKA, DAR ES SALAAM
Meya wa zamani wa Jiji
la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi amefikwa na umauti jana majira ya saa tatu
na nusu usiku katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa.
Taarifa za kifo chake
zimethibitishwa na ndugu yake, Dk. Makongoro Mahanga...
Muuza maji jela kwa kuiba mti

NA
MWANDISHI WETU
MAHAKAMA ya Mwanzo ya Ilala imemhukumu Muuza maji mkazi wa
Keko jijini Dar es Salaam Emmanuel Issa (38) kifungo cha miezi minane jela kwa
kosa la kuiba miti 12 aina ya mchikichi.
Akisoma hukumu hiyo Hakimu Asha Mpunga alisema mshtakiwa
alitenda kosa hilo...
Wednesday, October 12, 2016
Miaka 30 jela kwa unyang’anyi

NA MWANDISHI WETU
MKAZI wa Kinondoni kwa Manyanya
Stephano Focus ‘ Malenga Tyson’ (29) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na
Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini hapa baada ya kukiri kosa la unyang’anyi wa
kutumia silaha.
Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu
Mkazi Adelf Sachore...
Monday, October 10, 2016
HUKUMU YA AJABU; Ahukumiwa kifungo cha maisha mara mbili na miaka 14

Washtakiwa wa kesi ya kulawiti, wizi na kusambaza picha za
udhalilishaji Erick Mdemu (mbele) na Juma Richard (katikati) wakitoka katika
mahakama ya Wilaya ya Ilala chini ya ulinzi mkali baada ya kuhukumiwa kwenda
jela.
NA JABIR JOHNSON
MAHAKAMA ya Wilaya ya
Ilala...
Friday, October 7, 2016
‘Scorpion’ mtoboa macho kizimbani

NA JABIR JOHNSON
Salum Njewete 'Scorpion' akipelekwa katika karandinga la Jeshi la Magereza baada ya kesi yake kuahirishwa kutokana na upelelezi kutokamilika.
MWALIMU wa sanaa za
mapigano Salum Njewete (34) maarufu Scorpion na mkazi wa Yombo Machimbo amepandishwa...