Wednesday, August 21, 2024

Dream Maker, Betpawa yatimiza ndoto ya Eric Salema kupata Kisima cha Maji Makiwaru

 

Kijiji cha Makiwaru  kimepata Maji ya Kisima kwa ajili ya shughuli za kila siku ikiwamo matumizi ya ndani kama kupika, kuoga, kufua na kadhalika.

Changamoto ya muda mrefu imefikia ukomo  baada ya kijana mwenye umri wa miaka 26 anayefahamika kwa jina la Eric Salema mwenyeji wa kijiji hicho kilichopo Magharibi mwa Mji mdogo wa Sanya Juu mkoani Kilimanjaro, kutimiza ndoto yake kupitia mradi wa Dream Maker, Betpawa  kwa manufaa ya wanakijiji hao.

“BetPawa walijitolea kuja kunichimbia kisima cha maji, kwa ajili yetu sisi wananachi, ukweli ni kwamba yatatusaidia sisi kama mwananchi wa kijiji hiki, kutatua changamoto yetu kubwa tuliyokuwa nayo hapa. Changamoto ya maji ipo kubwa maji mabomba ya maji yapo lakini upatikanaji wa maji ni wa kusuasua, inaweza kupita wiki hatupati maji kabisa kupitia mradi huu unakwenda kutatua changamoo hiyo,” anasema Eric Salema.

Meneja Masoko wa Betpawa Bi. Borah Ndanyungu anasema Mradi wa Dream Maker ni njia ya kurudisha kitu kwa umma bila kujali ni mteja wa kampuni  hiyo au la.

“Tulipata ndoto zaidi ya 15,000 lakini ndoto ya Eric Salema ilitugusa zaidi, ndoto ambayo ni endelevu ambayo inaigusa jamii moja kwa moja na sisi kama kampuni tunatumia muda takribani mwezi ikiwa na tim u ya watu mbalimbali kupitia hizi ndoto za wananchi ambazo huziwasilisha kwetu,” anasema Borah Ndanyungu.

Eric anasema ndoto yake ilikuwa kweli baada ya kutembelea mtandao wa Betpawa ambao uliweka namna ya kufikia ndoto ni muhimu kuwasilisha wazo ambalo litakuwa na manufaa kwa wananchi.

Mhandisi wa Kisima hicho Injinia John Francis Madaraka anasema uzinduzi wa kisima hicho ambacho kimegharimu kiasi cha shilingi mil. 24 za Tanzania utahudumia wakazi kati ya 4000 hadi 6000.

“Tumechimba kina cha mita 90 maji ni safi na salama, yamesha thibitishwa tuliyapeleka Idara ya Maji  wakayapima yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ambapo kisima hicho kina uwezo wa kuhudumia watu kati ya 4000 hadi 6000,” anasema Injinia Madaraka.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Makiwaru Jackson Moye anasema changamoto ya maji kijijini hapo imekuwapo kwa muda sasa lakini ujio wa kisima hicho umepunguza huku akisifu juhudi za kijana Eric Salema.

“Kwa kipindi cha kiangazi maji huwa madogo, wananchi hulazimika kutafuta maji vituo vingine na wakati mwingine usiku wakitafuta maji, Mradi huu ambao umetufikia katika kijiji hiki, utakwenda kupunguza changamoto ya maji, tunashukuru sana kwa hiki kilichofanyika husasan kwa kijana wetu kwa kuchagua mradi huu uletwe hapa nyumbani kwa wazazi wake,” anaongeza Moye.

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kijiji cha Makiwaru kina wakazi 3425 hivyo uwepo wa kisima hicho chenye urefu wa mita 90 utaondoa kero ya wakazi wa kijiji hicho kusafiri umbali mrefu kutafuta maji.

Mradi wa Dream Maker katika msimu wake wa pili umegharimu kiasi cha shilingi mil. 600 kutimiza ndoto 20 zilizochaguliwa kati ya 10,000 zilizowasilishwa Betpawa kwa njia ya mtandao.







0 Comments:

Post a Comment