Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Mapambano dhidi ya Habari za Uongo hayapaswi kukoma

Habari za uongo, habari za uongo zinazosambazwa kwa lengo la kumdhuru mtu au jambo fulani, huifanya jamii kuwa na sintofahamu. Zinaweza kutumika kwa madhumuni ya kiitikadi, kisiasa au hata uhalifu, kama vile ulaghai mtandaoni unaolenga kuiba data ya kibinafsi.

Utandawazi na Athari zake katika Uandishi wa Habari

Katika jamii yetu ya kisasa, ambapo habari ziko kila mahali na zinaweza kupatikana kwa kila mtu, mara nyingi ni ngumu kutofautisha kati ya vyanzo vya kuaminika na habari bandia.

Uandishi wa Habari nguzo msingi mkuu kwa ujenzi wa jamii inayojitambua

JAIZMELA blog ni miongoni mwa vyanzo vya habari, zilizochakatwa kwa kuzingatia miiko ya uandishi wa habari.

Mila na Desturi ni nguzo muhimu

Mila na desturi ni nguzo muhimu sana katika utamaduni wa jamii yoyote ile; mila ni sawa na sheria zisizoandikwa. Mila ni taratibu za maisha na mwenendo zinazofuatwa na jamii fulani katika utendaji kulingana na historia na utamaduni wao. Mila zinatambulisha maadili ya jamii husika, huelezea namna jamii inavyoendesha mambo yake.

Tuesday, December 18, 2018

RON W. DAVIS: Namna alivyokuwa kocha wa Timu ya Taifa ya Riadha Tanzania-3


Ron W. Davis Novemba 2018 alikuja Tanzania kwa mara ya pili.
DAR ES SALAAM, TANZANIA
Makala yaliyopita tulijikita kuangazia maisha ya awali ya mwanariadha na mwanamapinduzi katika mchezo huo Ron William Davis na namna alivyopata nafasi ya kuzuru bara la Afrika. 

Aidha katika tuliangazia namna alivyokutana na mpiganaji wa taifa la Afrika Kusini Nelson Mandela mwanzoni mwa miaka ya 1990 ambaye alitumia mchezo wa riadha kuomba radhi wanamichezo wa Afrika Kusini ambao walifungiwa kushiriki michuano tangu mwaka 1960 kutokana na vitendo vya ubaguzi wa rangi. 

Tuliona Mandela alipopaza sauti yake kwa watu wa Afrika ya Kusini walimwelewa na ikawa sababu mojawapo iliyomfanya akalie kiti cha urais wa taifa hilo mwaka 1994 ikiwa ni miaka michache baada ya kutoka jela la Rhode Island alikodumu kwa miaka 27. 

Katika makala haya tutaangazia namna alivyotua Tanzania na kuwa kocha mkuu wa timu ya riadha ya taifa. Kwa ufupi Ron Davis ndiye kocha wa kwanza kuiletea Tanzania medali pale alipomsimamia mkongwe Filbert Bayi na Suleiman Nyambui katika mashindano ya kimataifa.

MICHUANO YA JUMUIYA YA MADOLA 1978
Mwaka 1978 michuano ya Jumuiya ya Madola ilifanyika mjini Edmonton, Alberta nchini Canada. Nigeria iliamua kuwa haitashiriki michuano hiyo kwani ilikuwa imetoka kwenye michuano ya All Africa Games ambayo Ron Davis alikuwa kocha huko. 

Sababu kubwa ya Nigeria ya kutoshiriki ilikuwa wazi kabisa kwa ilikuwa imegomea kuunga mkono michuano hiyo kutokana na New Zealand kushiriki mashindano ya michezo na taifa la Afrika Kusini wakati huo ubaguzi wa rangi ulikuwa wa kiwango cha juu. 

Kitendo hicho cha Nigeria kufanya hivyo hakikuwa kigeni kwani mwaka 1972 iliongoza mgomo wa michuano ya Olimpiki ilifanyika mjini Munich nchini Ujerumani pia ilifanya hivyo katika Michuano ya Olimpiki ya mwaka 1976 iliyofanyika Montreal nchini Canada. 

Katika mahojiano na Ron Davis anasema, “Nigeria ilikuwa na msimamo wa kuunga mkono mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi ambao ulikuwa ukienea kwa kasi, na juhudi hizo zilienea duniano kote.” Ron Davis analikumbuka vema tukio hilo la michuano ya Jumuiya ya Madola kwani taifa la Canada ambao walikuwa wenyeji wa mashindano hayo walipeleka ndege yao Air Canada nchini Algeria ambayo ilitumika kuchukua wanamichezo wa Afrika ambao walikwenda kushiriki. 

Kocha huyo anasema, “Mimi, Lee Evans na John Carlos hatukupanda ndege hiyo na timu lakini tulitumia ndege ya Ujerumani kwa ufadhili wa kampuni ya Puma, kwani Carlos alikuwa akiiwakilisha Puma katika michuano ya Jumuiya ya Madola.” 

Ron Davis anasema kuwa uwepo wa Carlos uliwafaidisha kwani baada ya siku kadhaa za kuwapo mjini Herzogenaurach miongoni mwa vitongoji mahiri katika jimbo la Bavaria nchini Ujerumani yeye na Carlos walikwenda Edmonton wakati Lee aliitwa California. 

Akiwa kwenye ndege Ron Davis anasema alikuwa haamini kama anakwenda kwenye michuano hiyo akiwa kama kocha na alitabasamu tu akikumbuka miaka ya nyuma ilivyokuwa katika kufikia ndoto zake. Canada haikuwa mara yake ya kwanza lakini safari ya kutinga katika michuano hiyo kama miongoni mwa makocha wakubwa duniani ndiyo ilimfanya atabasamu ndani ya ndege. 

Wakati naandika makala haya nikakumbuka nukuu ya mwanamitindo na mwigizaji wa kike wa Marekani Christie Brinkley aliposema, “Ishirikishe dunia na tabasamu lako. Ni alama ya mahusiano mazuri (urafiki) na amani.” 

Hakika hata sasa ukimuona Ron Davis tabasamu lake bado analo hiyo ikimaanisha ndiye yule aliyetabasamu ndani ya ndege ikimaanisha ni mtu wa amani. Na amani yake ndiyo ilimfanye akutane na ujumbe kutoka Tanzania katika michuano hiyo.

HATUA MOJA MBELE
Ron Davis akihojiwa na mwandishi wa habari Jabir Johnson Novemba 2018 Mkuza, Kibaha mkoani Pwani.
Ron Davis anasema, “Siku moja nikiwa katika mazoezi ya kukimbia, yoga na kujinyoosha katika njia za Chuo Kikuu cha Alberta wakati michuano hiyo ikiendelea nilienda kwa kocha wake wakati ambaye siku hiyo alikuwa na Filbert Bayi wakifanya mazoezi.” 

Aidha Ron Davis alikuwa hajui kwa wakati huo alipokutana na kocha wa Filbert Bayi kama ingetengeneza njia. Wakati huo kocha Sulus alikuwa akimnoa Bayi. Baada ya mazungumzo ya muda Sulus alimtambuliza kwa Waziri wa Michezo na Utamaduni wa Tanzania alikuwapo Edmonton. 

Hapo ndipo walipopanga muda mzuri wa kukutana ili kubadilishana mawazo na uzoefu kuhusu mchezo wa riadha. Ron Davis anasema alishtushwa na namna mwakilishi huyo wa nchi alivyomkaribisha kutokana na kwamba alikuwa bado ni kocha wa timu ya taifa ya Nigeria ingeleta mkanganyiko lakini alisubiri nini kitakachotokea.

Unafikiri nini kilifuata baada ya Ron Davis kukutana Kocha Sulus na Waziri wa Michezo na Utamaduni katika mashindano ya Jumuiya ya Madola mwaka 1978? Tukutane juma lijalo katika mwendelezo wa makala haya.

Makala haya yametayarishwa na Jabir Johnson ambaye alipata fursa ya kuzungumza na Ron Davis  katika masuala mbalimbali ya maisha yake na medani ya riadha alipotua nchini Tanzania. Pia yalichapishwa katika Gazeti la Tanzania Daima. Kwa maoni ushauri barua pepe: jaizmela2010@gmail.com

Wednesday, December 12, 2018

Lucas Moura aipeleka Spurs hatua ya 16 Ligi ya Mabingwa Ulaya

Lucas Moura akipongezwa na wenzake baada ya kuisawazishia Tottenham
Lucas Moura hawakuweza kuuzuia mkwaju ulipa Spurs kusonga mbele
Dakika ya 85 ya mchezo ubao wa matokeo Camp Nou ulibadilika baada ya Mbrazil Lucas Moura kuisawazishia Spurs
Heung Min Son litoa mchango wa bao hilo akimpita Thomas Vermalen katika mchezo huo.
Qusmane Dembele aliwashika kweli kweli Spurs ambapo dakika ya saba ya mchezo alipachika wavuni bao la kuongoza

Lionel Messi aliingia akitokea mechi akichukua nafasi ya Munir El Hadadi

Tuesday, December 11, 2018

Daei: Iran inaweza kukutana na Japan mataifa ya Asia 2019

Ali Daei

DEC. 11, 2018 - Mkongwe wa kandanda nchini Iran Alli Daei amesema taifa lake linaweza kukutana katika fainali na Japan katika michuano ya Mataifa ya Asia yanayotarajiwa kuanza Januari 5 kwenye ardhi ya Falme za Kiarabu. 

Daei anasema Japan ilionyesha mpira mkubwa katika Kombe la Dunia nchini Russia sawa na Iran. Hata hivyo nyota huyo anayeongoza kwa ufungaji wa mabao wa mashindano hayo akifunga mabao 14 katika mara tatu alizoshiriki akiwa na Iran amewataja nyota wa kikosi cha kocha Melli, Alireza Jahanbakhsh, Saman Ghoddos, Mehdi Taremi na Sardar Azmoun kuwa ni muhimu katika kuipeleka Iran fainali za michuano hiyo hapo mwakani. 

Iran ni mabingwa mara tatu wa Kombe la Mataifa ya Asia kwa mara ya mwisho ilitwaa taji hilo mwaka 1976.

Sunday, December 9, 2018

Uhuru wa Tanganyika 1961


Ramani ya Tanganyika, wakati wa Utawala wa Ujerumani; Tanganyika ilikuwa ikiitwa German East Africa (GEACO)
Taifa la Tanganyika lilijipatia uhuru wake Desemba 9, 1961 kutoka kwenye makucha ya Uingereza. Historia yake inaanzia mbali, harakati za kudai uhuru wa Tanganyika ambayo baadaye (1964) ilikuja kuungana na Zanzibar kuunda inayoitwa sasa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Mwandishi wa harakati za uhuru wa Tanganyika Mohammed Said katika kitabu chake cha “The Life and Times of Abdulwahiid Sykes,” anasema  Julius Kambarage Nyerere alikuja Dar es Salaam mwaka 1952 akiwa kama mwalimu wa shule ya St. Francis College, Pugu. 

Nyerere alikuwa na Mwapachu huko Tabora katika mwaka 1945, na Makerere College na baadaye nchini Uingereza wakichukua masomo ya juu. 

Inawezekana kwamba Nyerere kufuatia harakati za chama cha TAA, alisikia kuhusu Abdulwahid kupitia kwa Mwapachu alipokuwa bado yuko Uingereza. Mwapachu na Nyerere walikuwa wanafunzi katika Chuo cha Makerere wakati ambapo Kasella Bantu na Nyerere walifundisha katika shule moja, St. Mary's School huko Tabora.

Uhuru wa Tanganyika huwezi kuuzungumzia bila kumzungumzia Mwalimu Julius Kambarage Nyerere namna alivyopita hadi kufikia kushika madaraka makubwa ya kuliongoza taifa.

Nyerere alipata kusema kwamba, ilikuwa dhahiri yake kufundisha kwa muda kisha aingie kwenye siasa. Hatimaye Nyerere alifanywa kuukubali ule uongozi ambao Tanganyika Africans Association (TAA) ilimpa.

Shindano baina ya aliyekuwa rais, Abdulwahid na Mwalimu wa shule asiyefahamika, Julius Nyerere, lilifanyika kwenye Ukumbi wa Arnatouglo Aprili 17, 1953. Ukumbi huu ukienda ofisi ndogo za Chama chsa Mapinduzi mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam utaonyeshwa tu.

Nje ya duara la uongozi wa TAA ambao ulimpendekeza kugombea, Nyerere alikuwa mgeni kabisa kwa wote waliokuwa na haki ya kupiga kura.

Shughuli za kisiasa za Nyerere zilianza tangu siku hii. Hapa alikuwepo Nyerere, mgeni na mtu aliyekuwa hana historia ya kuongoza mapambano ya watu dhidi ya serkali ya kikoloni.
Familia ya Sykes ilikuwa imehusika na siasa za kienyeji mjini Dar es Salaam kwa takribani robo ya karne wakianzisha na kuongoza vyote viwili vyama vya African Association na Al Jamiatul Islamiyya. 

Abdulwahid kama mtoto wa Kleist Sykes alikuwa mmoja wa familia iliyojadili hadharani masuala ya kisiasa ya siku zile na kuyaandika wakati mwingine wakiandikiana barua na mamlaka ya kikoloni.

Uchaguzi ulikuwa wa kuinua mikono. Phombeah aliyekuwa mfawidhi wa Ukumbi wa Arnatouglo alikuwa msimamizi wa uchaguzi huo. Phombeah aliwaomba wote wawili Abdulwahid na Nyerere kutoka nje ya ukumbi ili uchaguzi uanze. 

Wiki nzima kabla ya uchaguzi Phombeah alikuwa akizunguuka huku na kule akimfanyia kampeni Nyerere. Lakini hakukuwa na haja ya kufanya hivyo, duara la ndani kabisa la TAA la Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz na Rupia lilikuwa tayari limekwishaamua kumfanya Nyerere awe rais wa chama.

Uchaguzi ilikuwa kutimiza utaratibu tu. Baada ya Abdulwahid na Nyerere kutoka nje upigaji kura ulianza Abdulwahid "alishindwa" uchaguzi huo ikiwa ni mara yake ya kwanza katika maisha yake yote ya siasa.
 
Bendera ya Tanganyika
Nyerere alishinda uchaguzi huo dhidi ya Abdulwahid aliyekuwa rais wakati huo kwa kura chache sana. Huu ulikuwa ndio mwanzo na mwisho kwa ushawishi wa familia ya Sykes katika chama cha TAA na mwanzo wa shughuli za kisiasa za Nyerere. Tangu siku ile historia ya kisiasa ya Tanganyika kamwe haikuwa ile ile tena.

Dossa Aziz alikuja kutoa taarifa kwamba Abdulwahid hakushindwa katika uchaguzi ule,
"Hakukuwa na namna yoyote Nyerere angeweza kumshinda Abdulwahid katika Dar es Salaam ya miaka ya 1950. Abdulwahid hakushindwa katika uchaguzi ule. Sisi sote tulitaka iwe vile. Uongozi wa TAA tulimtaka Nyerere."

Abdulwahid alikuwa mwenye kuonekana mara kwa mara, kama rais wa TAA aliifanya ofisi yake ipendeze. Alizoea kuwakaribisha watendaji wa TAA nyumbani kwake kwa chakula cha mchana na usiku na hili liliongeza umaarufu wake. Wakati huo wengi walidhani Nyerere asingefaa katika nafasi ile ya Abdulwahid.

Marehemu Tewa Said alipata kueleza kwamba siku ile kabla ya uchaguzi pale katika Ukumbi wa Arnatouglo, Abdulwahid alikwenda nyumbani kwake jioni. 

Wakati huo Tewa alikuwa akikaa mtaa wa Pemba si mbali sana toka nyumbani kwa Abdulwahid. Abdulwahid alimwambia Tewa haya kuhusu mabadiliko ya uongozi ambayo waliamua yafanyike kwenye chama cha TAA;

"Tewa, kesho tunakwenda kumpa huyu mtu, Nyerere, mamlaka ya kuendesha nchi hii. Kuanzia hapo, mara tu tutakapomchagua kutuongoza hakuna namna ya kumnyang'anya mamlaka hayo. Hatumfahamu vizuri sana lakini natumaini kila kitu kitakwenda vizuri." 

Tewa akikumbuka matukio yaliyopelekea Nyerere kuchaguliwa kama rais wa TAA alisema; "Kitu pekee alichokuwa nacho Nyerere zaidi ya Abdulwahid kilikuwa ile digrii ya chuo kikuu. Abdulwahid kwa takribani miaka minne tangu akamate ofisi katika mwaka 1950, alikataa kuitisha mkutano wa wajumbe kwa sababu moja au nyingine, mpaka alipokutana na Nyerere. Ninaamini kama Abdulwahid angekwenda Makerere tungeunda chama cha TANU mapema zaidi, labda kabla ya mwaka 1954 na Abdulwahid angekuwa rais, hata kama angeshindana na Nyerere."

Haya ni miongoni mwa mambo yaliyokuwapo nyuma ya uhuru wa Tanganyika ambayo mwaka 1919 sehemu kubwa ya koloni la Kijerumani ilikabidhiwa rasmi mikononi mwa Uingereza kama eneo la kudhaminiwa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa kulingana na kifungo 22 cha mkataba wa Versailles. 

Wajerumani walianza kushirikia eneo la Tanganyika tangu mwaka 1886 ikiwa ni miaka miwili baada ya Mkutano wa Berlin mwaka 1884.
Ramani ya Afrika