Wednesday, February 26, 2025

Kwanini Filbert Bayi bado yu vinywani mwa Wanigeria?

 

Mvuto wa riadha si kwamba ni mchezo pekee wenye usafi, haki, usahihi na uzuri; haiba yake halisi ni kwamba ni binadamu sana. Wakati wanariadha wanashindana dhidi ya wengine, kila mmoja anapigania kufanya bora kabisa dhidi ya udhaifu wao wenyewe. Baada ya kushinda basi historia na hadithi zinaweza kupatikana.

Unamkumbuka gwiji wa Nigeria na Mshindi wa Medali ya Dhahabu ya Olimpiki, Enefiok Udo Obong; mnamo mwaka 2020 alimzungumzia sana Bayi?

Kuna maswali mengi kuhusu Filbert Bayi gwiji wa riadha duniani kote kwanini Mtanzania huyu wa kwanza aliyeshinda medali ya dhahabu ya Olimpiki kuwa kinywani mwa Wanigeria?

Gwiji wa soka Patrick Olusegun Odegbami, ambaye mara nyingi hufupishwa kwa Segun Odegbami alijibu swali hili, kwa nini Wanigeria wanamzungumza na Bayi wakiwa bado hai,

 “Hadithi ya Filbert Bayi ni yenye changamoto na kutia moyo. Ni kwa wavulana na wasichana wote wa Kiafrika wenye ndoto ya kutumia vipawa vyao vya asili vya talanta, mazingira, kasi, uvumilivu na nguvu kushindana dhidi ya ulimwengu wote, na kuendeleza mchakato wa kuzaliana kwa vizazi vipya vya wanariadha wa Kiafrika, wa kiwango cha kimataifa, "alisema Odegbami.

Mnamo 1973, mwanariadha chipukizi mwenye umri wa miaka 20 kutoka Tanzania alifika kwenye All Africa Games iliyofanyika Lagos, Nigeria, ambako alitangaza kuwasili kwake kwa riadha ya kimataifa kwa kushinda medali ya dhahabu na kuweka rekodi mpya ya Kiafrika katika uwanja uliojumuisha mmoja wa wanariadha wakubwa zaidi ulimwenguni wakati huo - mshindi wa medali ya Dhahabu ya Olimpiki ya Kenya, Kipchoge Keino.  

Michezo ya 1973 ilikuwa michezo ya pili ya All-Africa Games iliyofanyika Lagos kuanzia Januari 7, 1973, hadi Januari 18, 1973. Nigeria ilichukua fursa hiyo baada ya kufanikiwa kwa Michezo ya kwanza ya Afrika, Kamati ya Maandalizi ya All Africa Games ilitoa nafasi ya jiji la Bamako, Mali kufanyika kwa mashindano hayo mnamo mwaka 1969.

Mapinduzi ya kijeshi yalivuruga mipango hiyo na waandaji wakahamishia michezo hiyo hadi Lagos, Nigeria ifanyike mwaka 1971.  

Michezo hiyo iliahirishwa kwa mara nyingine na hatimaye kufunguliwa Januari 1973. Mwenge uliwashwa mjini Brazzaville wiki moja kabla ya michezo na kusafirishwa hadi Lagos ikiwa ni ishara ya mwendelezo wa michezo hiyo.

Mwaka mmoja baadaye, Filbert Bayi akiwa na umri wa miaka 21, ambaye wakati huo alikuwa hajulikani sana nje ya Afrika, alifika ulimwenguni kwa kishindo.

Katika Michezo ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth Games) huko Christchurch, New Zealand, aliandika jina lake kwa dhahabu milele, kwa kuwashinda magwiji na miamba ya riadha wakati huo katika mbio za kati - Rod Dixon, Ben Jipcho, Mike Boit, Brendan Foster na John Walker.

Katika mbio hizo kuu za mbio za mita 1500 ambazo zilimfanya awe gwiji, Roger Bannister alikaririwa akisema  “Mbio kubwa kuliko zote ambazo nimewahi kuona”, Filbert aliharibu uwanja na kuvunja rekodi ya dunia, akikimbia umbali mzima kwa mtindo mpya wa kuvutia ambao ungekuwa alama yake ya biashara - akikimbia kwa kasi ya kutisha kutoka 'bunduki hadi tape', mbele ya pakiti!

Kwa muongo uliofuata, Filbert Bayi alikua mmoja wa wakimbiaji wanaozungumzwa zaidi, waliopendwa na wanaotafutwa sana ulimwenguni.

Odegbami ambaye alishinda mechi 46 na kuifungia timu ya taifa ya Nigeria mabao 23 ambayo aliiongoza hadi kutwaa taji lake la kwanza la Kombe la Mataifa ya Afrika katika michuano ya 1980 nchini kwao alisema, “Njia yangu na Filbert ilivuka mara kadhaa katika siku hizo ingawa hatukuwahi kukutana moja kwa moja. Tulikuwa kwenye Michezo ya Olimpiki ya 1976 huko Montreal, Kanada, kama sehemu ya wanariadha wachanga kutoka nchi 27 za Afrika walioondoka usiku wa kuamkia leo kupinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini.

"Tulikuwa pamoja pia kwenye Michezo ya All-Africa ya 1978 huko Algiers. Hatimaye, sote tulikuwa manahodha na washika bendera wa kikosi cha Olimpiki cha nchi zetu katika Michezo ya Olimpiki ya 1980 huko Moscow,” Odegbami aliongeza.

Bayi na Odegbami tangu walipostaafu michezo, wamepanga njia zinazofanana kwa kutengeneza urithi kwa kizazi kijacho kupitia uanzishwaji wa taasisi za maendeleo ya michezo na elimu kwa nchi zao.

Baada ya hadithi ya mafanikio mjini Lagos mwaka wa 1973, Bayi alitetea taji lake katika Michezo ya All-Africa ya 1978 iliyofanyika Algiers alitumia saa 3:36.21 akiwaacha Mkenya Wilson Waigwa (3:36:48) na Mualgeria Amar Brahmia (3:37:33).

Kwa sasa Bayi pia ni mjumbe wa Kamati ya Kiufundi ya IAAF na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki ya Tanzania.

Credit to: Jabir Johnson, Tanzanian Journalist/ JAIZMELA

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment