Saturday, February 1, 2025

Watatu wafariki dunia papo hapo kwa ajali mjini Moshi

 

Watu watatu wamefariki dunia kutokana na ajali iliyohusisha gari dogo na mabasi mawili ya Abiria mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, kwa kile kinasadikika ni mwendokasi na kuovertake.

Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro lilifika eneo la Kaanan, mjini hapa ilipotokea ajali hiyo kwa ajili ya uokoaji ambapo gari aina ya Toyota Rav 4 yenye namba za usajili T 592 EKU iligongana uso kwa uso na basi la Esta Luxury Coach tana na changamoto hiyo katika barabara ya Moshi- Arusha ikitokea Himo.

Mashuhuda wa tukio hilo wanasema mabasi ya abiria ya Kidia na Esta Luxury Coach ndio chanzo cha ajali hiyo baada ya Kidia kushindwa kumaliza kulipita gari la Esta ambapo Rav 4 ilikutana uso kwa uso na basi la Esta.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Godfrey Mzava amesema ajali hiyo ilitokea leo saa 12:30 asubuhi na kwamba abiria waliokuwepo katika basi la Esta walipatiwa basi jingine kuendelea na safari ya Dar es Salaam.

Miili ya Marehemu iliyokuwemo katika Rav 4 imehifadhiwa katika Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya KCMC kwa ajili ya uchunguzi zaidi na taratibu nyingine za mazishi.



0 Comments:

Post a Comment