Ukweli na Kuheshimiana ni kiini ujenzi wa jamii zetu

Ulimwenguni kwa sasa kumejaa habari potofu na upotoshaji, ni muhimu kuhakikisha kwamba ukweli na kuheshimiana vinakuwa kiini kwa ujenzi wa jamii zetu.

Mapambano dhidi ya Habari za Uongo hayapaswi kukoma

Habari za uongo, habari za uongo zinazosambazwa kwa lengo la kumdhuru mtu au jambo fulani, huifanya jamii kuwa na sintofahamu. Zinaweza kutumika kwa madhumuni ya kiitikadi, kisiasa au hata uhalifu, kama vile ulaghai mtandaoni unaolenga kuiba data ya kibinafsi.

Utandawazi na Athari zake katika Uandishi wa Habari

Katika jamii yetu ya kisasa, ambapo habari ziko kila mahali na zinaweza kupatikana kwa kila mtu, mara nyingi ni ngumu kutofautisha kati ya vyanzo vya kuaminika na habari bandia.

Uandishi wa Habari nguzo msingi mkuu kwa ujenzi wa jamii inayojitambua

JAIZMELA blog ni miongoni mwa vyanzo vya habari, zilizochakatwa kwa kuzingatia miiko ya uandishi wa habari.

Mila na Desturi ni nguzo muhimu

Mila na desturi ni nguzo muhimu sana katika utamaduni wa jamii yoyote ile; mila ni sawa na sheria zisizoandikwa. Mila ni taratibu za maisha na mwenendo zinazofuatwa na jamii fulani katika utendaji kulingana na historia na utamaduni wao. Mila zinatambulisha maadili ya jamii husika, huelezea namna jamii inavyoendesha mambo yake.

Tuesday, April 30, 2024

Miili ya Familia iliyosombwa mafuriko yaagwa KDC-Moshi DC

Miili ya Watu waliofariki kwa mafuriko wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro imeagwa leo asubuhi Aprili 30, 2024 katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya hiyo na Mamia ya waombolezaji.Tito Chaki (1961-2024), Joram Kimambo (2011-2024), Freddy Justus (2018-2024), Anjela Chaki...

Saturday, April 27, 2024

AMANI GOLUGWA: Maandamano ya Chadema sio Kelele, Sherehe au Picnic

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini Amani Golugwa akizungumza na waandishi wa habari siku chache kabla ya maandamano ya Aprili 30, 2024 mjini Moshi Kushoto ni Katibu wa Chadema Moshi Mjini Mzee Minja na Kulia ni Mwenyekiti wa Chadema na Mstahiki Meya Mstaafu Moshi Raymond Mboya....

Tuesday, April 23, 2024

Takukuru Kilimanjaro yabaini ‘madudu’ ujenzi Bweni Machame Girls

Mkuu wa Takukuru mkoa wa Kilimanjaro Mussa Chaulo akizungumza na vyombo vya habari mnamo Aprili 23, 2024 kuhusu utendaji kazi wa miezi mitatu kutoka Januari hadi Machi 2024 wa taasisi hiyo. Picha na JAIZMELASintofahamu ya ujenzi wa bweni katika Shule ya Sekondari ya wasichana...

Wednesday, April 17, 2024

Diaspora wa Msumbiji mkoani Kilimanjaro kupiga kura mjini Moshi Okt. 9, 2024

Raia wa Msumbiji waishio mkoani Kilimanjaro na maeneo mengine nchini Tanzania wametakiwa kujitokeza katika uchaguzi mkuu wa taifa hilo la Kusini mwa Afrika unaotarajiwa kufanyika Oktoba 9, 2024  Akizungumza na Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Kilimanjaro...

Thursday, April 11, 2024

Uwekezaji Shule ya Kibo Shanty, Moshi unavyomtesa Ibra Line; Jumuiya ya Wazazi yamwita 'Muhuni'

Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Kilimanjaro imethibitisha bila shaka yoyote kuwa mleta vurugu katika uwekezaji katika Shule ya Kibo Shanty ni mwanasiasa na mfanyabiashara maarufu  Ibrahim Shayo "Ibra Line".Aidha Jumuiya hiyo imesema kuwa Ibra...