Saturday, March 8, 2025

Mo Dewji bilionea wa 1588 duniani 2025, Tajiri pekee Orodha ya Forbes kutoka Tanzania

Kwa mujibu wa Forbes inasema tajiri namba moja nchini Tanzania Mohammed Dewji (49) maarufu Mo katika nafasi za mabilionea mwaka 2025 ni 1588.

Mo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa METL amekuwa akifanya kazi Afrika Mashariki na Kati katika nchi za Kenya, Ethiopia, Uganda na Tanzania.

Hadi tarehe 8 Machi 2025 Mo ametajwa kuwa na utajiri wa Dola za Kimarekani 2.2 bilioni ikimweka katika nafasi hiyo; Utajiri huo umepanda kutoka Dola la Kimarekani 1.8 bilioni Januari 2024 ukimweka wakati huo katika nafasi ya 12 barani Afrika.

Mnamo mwaka 2016 ndiye Mfanyabiashara pekee nchini Tanzania alisaini Giving Pledge akitoa ahadi ya kujitolea walau nusu ya utajiri wake kwa ajili ya wenye mahitaji (philanthropic causes).

Kama ilivyo kwa wafanyabiashara wengine, ushindani ni suala la muhimu; Mo ameendelea kutoa ushindani kwa makampuni kama Coca Cola kwa kuzalisha kinywaji kipya cha Mo Cola.

Mpaka sasa Mo Dewji ndiye mtanzania pekee aliyepo kwenye orodha ya mabilionea wa dunia

Kwa mujibu wa Forbes, Elon Musk, Mark Zuckeberg na Jeff Bezos wanashika nafasi za juu za mabilionea duniani.

Wakati huo huo Forbes imemtaja Rais wa Shiriksho la Soka Barani Afrika Patrick Motsepe (63) kuwa ni Bilionea wa 1173.

Utajiri wa Motsepe wa Dola za Kimarekani 3 bilioni unafanya katika taifa lake la Afrika Kusini kushika nafasi ya nne akizidiwa na Koos Becker ambaye duniani anashika nafasi ya 1049, Nick Oppenheimmer & family nafasi ya 254 na tajiri namba moja nchini Afrika Kusini Johann Rupert & family anayeshika nafasi ya 164.

Aidha ni matajiri sita pekee kutoka Afrika Kusini ambao wapo katika orodha ya mabilionea wa dunia wa Forbes.

Credit to: Jabir Johnson/JAIZMELA/Forbes.

Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment