Monday, January 27, 2025

Yuji ‘Gump’ Suzuki awasili Cape Town (SA) kwa mguu, baada ya siku 210

Yuji "Gump" Suzuki mnamo Januari 26, 2025 jijini Cape Town baada ya kuwasili akihitimisha safari yake ya kilometa 6,000 kutoka Nairobi, Kenya. Yuji alitumia miezi saba kutoka Juni 2024 hadi Januari 26, 2025.


“Hayo ni Maisha Yangu”; alisikika Mjapan mmoja akitamka mnamo Januari 26, 2025 katika viunga vya jiji la Cape Town nchini Afrika Kusini baada ya kuwasili akitokea Nairobi, Kenya kwa mguu.

Cha kustaajabisha ni kwamba Mjapan huyo aliyefahamika kwa jina la Yuji ‘Gump’ Suzuki aliwasili katika jiji hilo lililo umbali wa kilometa 6,400 kutoka Nairobi, Kenya akiwa na mkokoteni wa matairi mawili akiongozana na vijana wengine wawili wa Kijapan.

Mjapan Yuji mwenye umri wa miaka 34 aliwasili jijini Cape Town humo akitumia siku 210 sawa na takribani miezi saba tangu alipoianza safari yake mnamo Julai 2024, alipita nchini Tanzania, Zambia, Zimbabwe na Namibia kabla ya kuingia Afrika Kusini.

Mapema asubuhi ya Januari 26, 2025 akiwa na mkokoteni wake uliojizolea umaarufu mkubwa wa ‘Rickshaw’ wenye uzito wa kilogramu 100; Yuji aliukokota kwa furaha na kuwapongeza vijana wenzake kwa kumuunga mkono katika safari hizo za kitalii

Nisingeweza kufanya bila ninyi ndugu zangu, ninatembea kwa furaha, nimekuwa nikisafiri kwa miaka tisa sasa na nimekuwa nikiungwa mkono nanyi hivyo narudisha kwenu. Hayo ni maisha yangu,” alisema Suzuki.

Yuji aliongeza kuwa changamoto za barabarani kubwa lakini iliyokuwa ngumu zaidi ni ya kupenya Jangwa la Namibia.

Kwa mujibu wa tovuti yake; mnamo mwaka 2016-2017 Yuji Suzuki; alitembea kutoka China hadi India pia kilometa 2,500 alizunguka barani Ulaya mnamo mwaka 2017; pia kilometa 5,100 nchini Marekani kati yam waka 2022-2023.

Mkokoteni wa magurudumu mawili (Rickshaw) ulianza kutumika lini?

Rickshaw ya kwanza ilivumbuliwa nchini Ufaransa mwishoni mwa karne ya 17; kwa ajili ya mahitaji ya usafiri licha ya uwepo wa aina nyingine za vyombo vya usafiri. Miaka hiyo ya 1679 Ufaransa ilikuwa imeendelea sana katika masuala ya usafiri  aina ya “Omnibus” ambazo zilikuwa zinafanana na waendeshaji wa mikokoteni ya kuuza mvinyo katika mitaa ya jiji la Paris. Wakati huo mikokoteni hiyo ilikuwa ikisukumwa na watu wawili mmoja anakuwa mbele akivuta na mwingine nyuma akisukuma. Huyu wa mbele alikuwa akishikilia mbao fulani ikiwa ni sehemu ya kutafuta mizania na kuongoza uelekeo anaoutaka.

Wasanii wa uchoraji hawakuwa nyuma Msanii Claude Gillot alichora picha yake aliyoipa jina la “Les deux carosses” ambao ulionyesha mikokoteni hiyo miwili; mchoro huo aliuchora mnamo mwaka 1707.

Katika ardhi ya Japan, wao walivumbua kivyao mnamo mwaka 1869 ambapo kipindi cha utawala wa Tokugawa (1603-1868) kulipigwa marufuku ya matumizi ya vyombo vya usafiri vinavyotumia matairi ikiwamo mikokoteni. Wakati mikokoteni ya Rickshaw ikianza ndio kipindi ambacho Japan ilikuwa imeanza kukua katika masuala ya ufundi.

Izumi Yosuke anasalia kuwa mvumbuzi wa kwanza wa Rickshaw nchini Japan akishirikiana na Suzuki Tokujiro na Takayama Kosuke ambao wote kwa pamoja walipata wazo kutokana na namna magari ya Farasi yanavyofanya kazi, miaka michache baadaye waliyaingiza mitaani na kuwa sehemu ya maisha kisha kusambaa hadi China na kwingineko.

Credit to: Jabir Johnson/ JAIZMELA/Mashirika ya Habari/Wikipedia 

+255 693 710 200






 

Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment